Auliwa na Robot nchini Korea Kusini
Mwanaume mmoja nchini Korea Kusini amekutwa na mauti baada ya kukandamizwa na Roboti linalofanya kazi kwenye kiwanda cha kupakia mboga.
Polisi wameanza uchunguzi wa kisa hicho kubaini ikiwa roboti hilo halikuwa salama ama lilikuwa na hitilafu.
Kwa mujibu wa polisi, mwanaume huyo alifariki kutokana na majeraha ya kichwani na kifuani, baada ya kushikwa na kukandamizwa kwenye mkanda wa kusafirisha mizigo na mikono ya roboti.
Kiwanda hicho kinatumia maroboti mawili kwa ajili ya kubeba mabox yaliyopakiwa mboga mboga za kusafirishwa nje ya nchi.