Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Kenya: Wanafunzi wahitimisha masomo ya elimu ya msingi katika mfumo wa 8-4-4

Kabla ya kukamilika kwa Alhamisi hii, wanafunzi zaidi ya milioni moja nukta mbili nchini kenya watakuwa wameshapata matokeo yao ya mtihani wa kitaifa wa darasa la nane unaofahamika kwa kiingereza kama {Kenya Certificate of Primary Education} KCPE.

Waziri wa Elimu nchini Kenya Ezekiel Machogu ametangaza mapema Alhamisi matokeo ya mtihani huo, baada ya kuwasilisha ripoti ya matokeo hayo kwa Rais William Ruto kama ilivyo ada ya shughuli za mitihani nchini humo.

Kwa wanafunzi waliokuwa watahiniwa mwishoni mwa mwezi Oktoba, bila shaka hali ya tumbo joto imejaa miyoni mwao, kila mmoja akiomba kwamba ametimiza angalau alama 250 kati ya mia tano ili kujipatia nafasi katika shule ya upili nzuri.

Waziri Machogu, anatekeleza kibarua cha pili tangu serikali ya Rais Ruto kuchukuwa uongozi nchini Kenya, ila matangazo haya ni muhimu katika historia ya elimu nchini humo kwa kuwa darasa la nane mwaka wa 2023, ndio la mwisho kabisa katika mfumo wa elimu wa 8-4-4 ambao umekuwepo tangu 1984, wengine wetu tulipozaliwa.

Kwa miaka 39, Kenya imetumia mfumo huo wa elimu ambapo wanafunzi wanasoma miaka minane katika shule ya msingi, minne katika shule ya upili na miaka minne kwenye chuo Kikuu, huku wanaojiunga na vyuo anuwai au taasisi za cheti cha stashahada wakisomea kwa muda wa kati ya miaka miwili na mitatu.

Ukitazama historia ya taifa hili ni kwamba Kenya imekuwa na mifumo kadhaa ya elimu tangu nyakati kabla ya ukoloni ambapo Waafrika walitumia mbinu mbali mbali za kufunza vizazi vinavyokua jinsi ya kuishi na kutekeleza majukumu kama vile ya nyumbani, shambani, sokoni, na hata jinsi ya kuishi katika jamii.

Waarabu walipoingia katika pwani ya Kenya, vyuo vya kidini almaarufu Madrassa vilitumika kutoa mafunzo ya kidini kwa jamii, ili kuwapa elimu ya ziada kando na iliyotolewa na jamii zao.

Vitabu vya historia vimenakili, kwamba masomo ya msingi nchini yalianzishwa katika hali hiyo hiyo Pwani ya Kenya wakati wamisheni walipoingia Kenya mnamo 1946.

Dkt Ludwig Kraf, mmishonari kutoka Ujerumani alianzisha shule ya kwanza Kenya huko Rabai, karibu na Mombasa na masomo yaliangazia kusoma, kuhesabu na kuandika.

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.