Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Misri kuwezesha uhamisho wa watu 7,000 wa kigeni kutoka Gaza

Misri kuwezesha uhamisho wa watu 7,000 wa kigeni kutoka Gaza

Misri inataka kuwezesha uhamisho wa wageni 7,000 walio na uraia kutoka nchi 60 huko Gaza kupitia kivuko cha ardhini cha Rafah.

Hatua hiyo ilijadiliwa wakati wa mkutano uliofanyika na maafisa wa Misri na mabalozi na wawakilishi wa nchi za nje jana, Jumatano.

Mamlaka ya Palestina ilichapisha orodha ya pili ya majina ya takribani raia 600 wa kigeni, wakiwemo raia 400 wa Marekani, ambao wataruhusiwa kuvuka kuingia Misri kuanzia leo.

Misri pia ilijadili maandalizi ya kupokea Wapalestina waliojeruhiwa na juhudi za Misri kuleta msaada.

Misri ilipokea Wapalestina 46 waliojeruhiwa kati ya 81, ambao walihamishiwa katika hospitali za Sheikh Zuweid, Al-Arish, na Bir Al-Abd.

Kivuko cha Rafah kilifunguliwa jana, Jumatano, kwa idadi ndogo ya majeruhi, wageni, na wenye hati za kusafiria za kigeni kuvuka, kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa vita.

Chanzo:Bbc

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.