Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

Mzunguko wa HEDHI kuathiri uwezo wa Mwanamke kubeba Mimba

Mzunguko wa HEDHI kuathiri uwezo wa Mwanamke kubeba Mimba

• • • • •

JE MZUNGUKO WAKO WA HEDHI UNAWEZA KUATHIRI UWEZO WAKO WA KUBEBA MIMBA?

Hili ni swali ambalo baadhi ya wanawake hujiuliza sana hasa wakiwa na matatizo katika mizunguko yao ya hedhi pamoja na tatizo la kutokubeba mimba,

Ukweli ni kwamba mzunguko wako wa hedhi unaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa tatizo la wewe kutokubeba mimba,

Hapa nazungumzia wanawake ambao wana matatizo mbali mbali kwenye mzunguko wa hedhi kama vile;

✓ Mzunguko wa hedhi ambao hubadilika badilika au usio kuwa na siku maalumu yaani kwa kitaalam tunaita Irregular menstrual cycle

✓ Kuchelewa sana kupata siku zao za hedhi,mfano kwa baadhi ya wanawake huweza kukaaa miezi miwili,mitatu N.k pasipo kuona hedhi

✓ Kublid damu nyingi na kwa muda mrefu bila kukata mfano zaidi ya wiki moja mtu anablid

✓Na ambao kila wakipata hedhi huonyesha dalili ya maambukizi ya magonjwa mengine kama vile; Mwanamke kupata hedhi ambayo inaenda sambamba na kuvimba mwili,miguu N.k,

hedhi inayoenda sambamba na kichefuchefu pamoja na kutapika sana

hedhi inayoenda sambamba na kuumwa sana hadi kufikia hatua ya kulazwa hospital N.k

Hivo wanawake wenye matatizo haya hata uwezo wa kubeba mimba huweza kuwa mdogo,

– lakini pia wengine hawajui kuhesabu siku za hatari katika mzunguko wao wa hedhi, hivo kufanya mapenzi siku ambazo hata ujauzito hawawezi kupata,

Kumbuka kuna aina kuu tatu ya mizungo ya hedhi kwa wanawake Mfano

• Mzunguko mfupi ambao ni mzunguko wa siku 21

• Mzunguko wa wastani ambao ni Mzunguko wa siku 28

• Na mzunguko mrefu ambo ni Mzunguko wa siku 30,33, 35 N.k

HITIMISHO; hivo kwa kuhitimisha, kutokana na maelezo niliyoyatoa hapo juu, ni kweli kwamba mzunguko wa hedhi huweza kuathiri uwezo wa mwanamke kubeba mimba

fahamu pia; Kuna asilimia chache sana ya wanawake ambao huweza kubeba mimba wakiwa katika siku zao za hedhi.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.