Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

TV 15 zaibwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Anthony Mtaka amemuelekeza Katibu Tawala wa Mkoa huo kuwasimamisha kazi baadhi ya Watumishi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe akiwemo Katibu wa Afya, Watu wa Idara ya manunuzi pamoja na Idara ya TEHAMA ili kupisha uchunguzi wa tuhuma za wizi wa TV 15 pamoja na kompyuta tatu katika Hospitali hiyo.

Mtaka ametoa maagizo hayo mara baada ya kushtukiza katika Hospitali hiyo baada ya kupata taarifa ya upotevu wa vifaa hivyo vilivyopotea miezi mitano iliyopita huku akimtaka Afisa manunuzi wa Hospitali hiyo Aloyce Kavumika kulipa takribani shilingi milioni.11 kwa ajili ya kununua TV 15 zilizoibwa.

Awali Afisa manunuzi akitoa taarifa ya wizi huo alisema alipata taarifa ya wizi wa TV July 08,2023 akiwa nje ya ofisi ambapo baada ya kurejea ofisini hapo alilazimika kukaa na Watumishi wenzake kwa nyakati tofauti huku wakikubaliana Watumishi wa Idara hiyo kuingia gharama zao kulipa TV hizo.

Amesema baada ya makubaliano hayo walikwenda kwenye moja ya duka la Mfanyabiashara mmoja mjini Njombe na kuagiza TV nyingine ambazo walipewa kwa makubaliano ya kuzilipa baada ya miezi miwili yaani mpaka mwezi huu wa November na waliweza kupewa bila maandishi yoyote kwakuwa wamekuwa wakishirikiana katika shughuli mbalimbali ambapo mpaka sasa fedha hiyo pia bado haijalipwa kwa mwenye duka.

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.