Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Mlipuko waua watu 8 na kujeruhi 84 Guinea

Mlipuko waua watu 8 na kujeruhi 84 Guinea

Takriban watu wanane wameuawa na wengine 84 wamejeruhiwa kufuatia mripuko mapema leo katika bohari ya mafuta katika mji mkuu wa Guinea, Conakry.

Takriban watu wanane wameuawa na wengine 84 wamejeruhiwa kufuatia mripuko mapema leo katika bohari ya mafuta katika mji mkuu wa Guinea, Conakry. Hayo yameelezwa na afisa mkuu wa polisi nchini humo ambaye amesema idadi hiyo ni ya muda na kwamba moto huo umedhibitiwa.

Mlipuko katika bohari pekee ya mafuta katika taifa hilo la Afrika Magharibi, ulitikisa wilaya ya Kaloum katikati mwa jiji la Conakry, na kuwalazimisha mamia ya watu kulikimbia eneo hilo.

Moto mkubwa na moshi mweusi vilishuhudiwa hadi kwa umbali wa kilometa kadhaa huku vikosi vya zima moto vikiwasili na malori ya mafuta yakiondoka eneo hilo yakisindikizwa na polisi. Serikali ya Guinea imewataka raia wa mji mkuu kusalia majumbani mwao.

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.