Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Burundi yafunga mipaka yake dhidi ya Rwanda

Burundi imesema imefunga mpaka wake na Rwanda, ikiwa ni wiki mbili sasa baada ya kulituhumu taifa hilo jirani kuwaunga mkono waasi waliofanya mashambulizi nchini humo.

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Burundi Martin Niteretse amesema uamuzi huo umeafikiwa baada ya kubaini kuwa, Rwanda inawahifadhi wahalifu wanaowashambulia Warundi. Madai ambayo Kigali imekuwa ikiyakanusha.

Kundi la RED-Tabara linashtumiwa kuendesha mashambulizi makali katika taifa hilo la Afrika Mashariki.Tangu 2015 kundi hilo halikuwa likifanya mashambulizi lakini tangu Septemba 2021, limekuwa likifanya mashambulizi kadhaa, ikiwa ni pamoja na dhidi ya uwanja wa ndege wa jiji kuu la Bujumbura.

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.