Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Mtoto wa Mr.Ibu aiba Michango ya Matibabu ya baba yake

Mtoto wa Mr.Ibu aiba Michango ya Matibabu ya baba yake.

Polisi nchini Nigeria wamemkamata mtoto wa kiume na mtoto wa kike wa kuasili wa mwigizaji maarufu wa vichekesho nchini Nigeria John Okafor, maarufu Mr Ibu, kutokana na madai ya kuiba pesa zilizokusudiwa kwa matibabu ya mwigizaji huyo.

Onyeabuchi Okafo na Jasmine Okekeagwu wanadaiwa “kumiliki simu ya mwigizaji huyo na kuingia katika mfumo wa benki”, kabla ya kuiba Naira milioni 55 sawa na dola $60,700.

Pesa hizo ni sehemu ya fedha ambazo zilikuwa zikichangwa na mashabiki na watu wenye mapenzi mema kwa ajili ya matibabu ya mwigizaji huyo, baada ya kuugua kwa muda mrefu mwaka jana.

Ugonjwa huo ulisababisha kukatwa kwa mguu mmoja wa Okafor.

Via:bbcswahili

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.