Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

Ugonjwa wa mang’ondi ni ugonjwa gani?

Ugonjwa wa mang’ondi ni ugonjwa gani?

Ugonjwa wa mang’ondi; ni neno ambalo ni maarufu sana kwa Jamii ya Wasukuma, lakini wanachomaanisha ni ugonjwa wa bawasiri,

Hivo ugonjwa wa mang’ondi ni ugonjwa wa bawasiri.

NB: Popote ambapo utaona tumeandika “ugonjwa wa mang’ondi” ujue tunamaanisha ugonjwa wa bawasiri. Na wenzetu wanaoelewa Ugonjwa wa mang’ondi ujue tunaelezea ugonjwa wa bawasiri.

Bawasiri ni nini?

Bawasiri, inayojulikana pia kama “piles au hemorrhoids,” inahusisha uvimbe na kutuna kwa mishipa ya damu katika njia ya haja kubwa, ikisababisha changamoto wakati wa kutoa kinyesi au kujisaidia haja kubwa.

Ugonjwa wa bawasiri huweza kumpata mtu wa jinsia yoyote(mwanaume&mwanamke)

Aina za Ugonjwa wa Bawasiri:

Kuna aina mbili kuu za bawasiri:

  1. Bawasiri za Ndani
  2. Bawasiri za Nje

Sababu za Ugonjwa wa Bawasiri:

Ingawa chanzo kamili cha ugonjwa wa bawasiri hakijulikani, wataalamu wa afya mara nyingi huzungumzia mambo kadhaa yanayochangia kutokea kwa bawasiri ikiwemo:

1. Kuwa na shida ya kupata Choo kigumu hasa ikiwa kwa muda mrefu(chronic constipation)

2. Kujitahidi,kujikaza au kutumia nguvu sana wakati wa kutoa kinyesi

3. Kuketi chooni kwa muda mrefu

4. Bawasiri pia inaweza kutokea kutokana na shughuli za kimwili kama vile;kunyanyua vitu vizito, vikisababisha shinikizo zaidi kwenye eneo husika.

Viashiria vya Hatari vya kupata Ugonjwa wa bawasiri;

Baadhi ya mambo yanayoongeza hatari ya kuwa na bawasiri ni pamoja na:

  • Ujauzito, kutokana na shinikizo kubwa la tumbo
  • Shida hii kuwa Zaidi kwenye familia
  • Uzito Mkubwa
  • Kupata Choo kigumu mara kwa mara n.k

Kutambua Ugonjwa wa Bawasiri:

Kufahamu dalili za Ugonjwa wa bawasiri ni muhimu. Ishara na dalili ambazo huonekana sana ni pamoja na:

– Kuwashwa sehemu ya haja kubwa

– Kutokwa na damu wakati wa haja kubwa

– Kuwa na Uvimbe au kutokeza kwa Kinyama sehemu ya haja kubwa

– Kuhisi kuchomwa au mchanga sehemu ya haja kubwa n.k

Ni muhimu kutofautisha maumivu ya bawasiri na matatizo mengine kama vile michubuko au proctitis.

Uchunguzi na Vipimo:

Wataalamu wa afya hufanya uchunguzi wa kina kwa kutumia anoscope, kifaa maalum kinachoingizwa sehemu ya haja kubwa, ili kuona hali ya njia ya haja kubwa na kutambua kama una Ugonjwa wa bawasiri au la!

Pia kupitia dalili na Ishara alizonazo mgonjwa huweza kusaidia kuitambua bawasiri kwa haraka.

Tiba na Mabadiliko ya Maisha:

Matibabu ya Ugonjwa wa bawasiri yanaweza kufanyika nyumbani au hospitalini. Mabadiliko ya maisha, kama vile kuongeza unywaji wa maji na lishe yenye wingi wa nyuzi nyuzi, ni muhimu kwako.

Ongeza matunda, mboga, na nafaka nzima kwenye lishe.

Fikiria virutubisho vya nyuzi nyuzi kama vile psyllium au methylcellulose kama lishe haijatosheleza.

Hakikisha unakunywa maji ya kutosha, angalau glasi sita hadi nane kwa siku.

Ushauri wa Kitaalam:

Kwa ushauri Zaidi, elimu, au matibabu, wasiliana nasi kupitia +255758286584. Tupo hapa kukusaidia.

Hitimisho:

Kuelewa chanzo, dalili, na chaguzi sahihi za matibabu ya ugonjwa wa bawasiri kunawawezesha watu kushughulikia na kuzuia tatizo hili kwa ufanisi. Jisikie huru kuwasiliana nasi kwa msaada zaidi na taarifa.

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.