Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Elimu&Ushauri

Kuvu nyeusi ni nini?, Na je Zina athari kwetu?

Kuvu nyeusi ni nini?, Na je zina athari kwetu?

Kuvu (mold), pia inajulikana kama scum, ni uyoga ambao hukua katika maeneo yenye unyevu.

Vijidudu vya kuvu viko kila mahali na kuna maelfu kwa maelfu katika angahewa ya dunia.

Ishara za kuvu ndani ya nyumba ni alama nyeusi, nyeupe au kijani-kama manyoya kwenye kuta na harufu mbaya na unyevu.

Je, kuvu nyeusi huathiri afya zetu na ni nini dalili zake?

Watu wanaoishi katika maeneo yenye kuvu wana uwezekano mkubwa wa kuugua magonjwa ya kupumua, maambukizo, mzio, na pumu au kushindwa kupumua.

Kuvuta pumzi au kugusa spora zinazotolewa na kuvu angani husababisha hisia kama vile kupiga chafya, makamasi, macho mekundu na kuwashwa na uharibifu wa ngozi.

Kuvu husababisha matatizo ya kupumua na kukohoa.

Kulingana na Taasisi ya Utafiti wa Makazi ya Uingereza, kila mwaka huduma ya afya ya umma ya Uingereza hutumia zaidi ya pauni bilioni moja kutibu magonjwa yanayosababishwa na kuishi katika nyumba zenye baridi na unyevunyevu.

Wazee, watoto na watoto wachanga, pamoja na watu walio na magonjwa ya kupumua na matatizo ya ngozi wako katika hatari za kuathiriwa na kuvu kuliko wengine.

Ni nini husababisha kuvu na inaondolewa kwa njia gani?

Uongofu wa gesi kwa maji ni sababu kuu ya kuvu.

Mara nyingi, kuvu hutokea katika sehemu za nyumba ambazo zina unyevu zaidi, kama vile bafu na vyoo, jikoni, na karibu na madirisha.

Wakati hali ya hewa inakuwa baridi, mvuke wa maji hubadilika kuwa matone ya maji na kukaa kwenye maeneo ya ndani ya nyumba ambazo zina joto chini ya kiwango cha umande.

Maeneo haya yanaweza kuwa kuta au madirisha yasioingiza mwanga vizuri.

Ikiwa hili halishughulikiwa kwa wakati, maeneo haya yatakuwa na unyevu hali inayoweza kuwa mazingira ya kukua kwa kuvu.

Nyumba za zamani na zile ambazo hazina mwangaza vizuri ziko katika hatari zaidi ya kuwa na kuvu.

Kuvu pia inaweza kutokana na shughuli za kila siku za nyumbani ambazo hutoa unyevu kupita kiasi, kama vile kuoga, kupika, na kukausha nguo katika eneo lililofungwa.

Kuoga kwa muda mfupi zaidi na kukausha maeneo yenye unyevunyevu, uingizaji wa hewa wa kutosha, kufungua madirisha ya jikoni na kutumia feni wakati wa kupika kutasaidia kuzuia ukuaji wa kuvu.

Ukarabati wa mabomba na mifereji ya maji yanayovuja pia ni muhimu ili kuzuia kuvu.

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.