Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo sababu mbali mbali zinazosababisha tatizo hili ambazo tutazichambua hapa,

Sababu zingine ni za kawaida, na zingine zinahitaji matibabu ya haraka. Tatizo la mate kujaa mdomoni huweza kuwa la muda mfupi au la kudumu.

Chanzo cha tatizo la mate kujaa mdomoni

Hizi hapa ni baadhi ya Sababu za tatizo hili la mate kujaa mdomoni;

– Tatizo la Kuzalishwa kwa mate kupita kiasi Mdomoni, au kwa kitaalam Hypersalivation,

Tatizo hili pia hujulikana kama sialorrhea au ptyalism, Na huhusisha mdomo kuzalisha mate mengi sana kupita kawaida.

Kulingana na sababu, tatizo la hypersalivation linaweza kuwa la mara kwa mara au kwa vipindi. Linaweza pia kuwa la muda mrefu au sugu.

Kwa wastani, mtu mwenye afya njema hutoa kati ya lita 0.75 na 1.5 za mate kila siku. Uzalishaji wa mate huongezeka wakati mtu anakula na huwa chini kabisa wakati wa usingizi.

Mate yakiwa mengi yanaweza kusababisha matatizo ya kuzungumza na kula, pamoja na midomo kupasuka au chapped lips na maambukizi ya ngozi.

Tatizo hili pia linaweza kusababisha wasiwasi kwa mtu,kutokujiamini kwa watu na kupunguza Mtu kujithamini.

– Sababu Zingine ni pamoja na;

(1) Madhara ya kuvaa meno bandia

(2) Matatizo kwenye muundo wa meno au Mdomo

(3) Kushindwa kumeza mate vizuri,au kuondoa mate mdomoni

(4) Kushindwa kuweka mdomo wako ukiwa umefungwa

(5) Hali ya Ujauzito ambayo huweza kusababisha mate kuzalishwa zaidi mdomoni

(6) Kuwa na maambukizi kwenye eneo la mdomo,ulimi au kinywa kwa ujumla,

Maambukizi makali kama ya Kichaa cha mbwa(rabies) au ugonjwa wa TB(tuberculosis)

(7) Tatizo la false teeth

(8) Kuwa na vidonda au Uvimbe mdomoni

(9) kupata matatizo ya Taya, mfano; Taya kuvunjika,kuhama mahali pake n.k

Ukiwa unatatizo hili hakikisha unapata msaada wa matibabu mara moja

AU KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.