Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

FAHAMU VYANZO VYA TATIZO LA MAUMIVU YA SHINGO NA MGONGO

SHINGO NA MGONGO

• • • • • •

FAHAMU VYANZO VYA  TATIZO LA MAUMIVU YA SHINGO NA MGONGO


 Tatizo hili huwasumbua baadhi ya watu wake kwa waume na zaidi ni watu wazima. Tatizo huwapata zaidi watu wa umri wa kati, yaani miaka 35 hadi 45 na huwa makali zaidi katika umri zaidi ya miaka 45.


Kazi ambayo mtu anaifanya huchangia kwa kiasi kikubwa hali hii ya maumivu. Zipo sababu mbalimbali zinazochangia hali hii ya maumivu ambazo tutakuja kuziona.


CHANZO CHA MAUMIVU

Maumivu ya shingo na mgongo hutokana na matatizo kwenye mishipa ya fahamu inayotokea katika uti wa mgongo. Mishipa ya fahamu inasimamiwa na uti wa mgongo na ubongo.


Matatizo katika ubongo husababisha maumivu makali ya kichwa na shingo na mambo yanayochangia ni malaria, homa ya uti wa mgongo, uvimbe kwenye ubongo na kuumia kichwa kutokana na ajali ya aina yoyote.


Maumivu ya shingo na mgongo husababishwa na maambukizi kama yale ya kichwani, mfano malaria na homa ya uti wa mgongo, uvimbe shingoni, kuumia shingo na mgongo, uvimbe, kufanya kazi ya kuinama kwa muda mrefu. Hali hii huwatokea zaidi watu wanaobeba vitu vizito kichwani, wanaokaa kwenye kiti muda mrefu na kiti ambacho hakipo katika kiwango kizuri cha kufanya mgongo na shingo vikae vizuri.


Kuumia pia kunaweza kusababishwa na gari kufunga breki ghafla na endapo hujafunga mkanda na kiti hakina ‘brace’ ya kusaidia kichwa, hivyo shingo itatikiswa kwa nguvu. Vilevile unaweza kuumia kwa kugonga kichwa sehemu ngumu, mfano kwenye bwawa la kuogelea au sehemu nyingine yoyote, kulala vibaya pia kunaweza kukusababishia uamke ukiwa na maumivu ya shingo na mgongo.


Uwepo wa magonjwa kama kisukari na shinikizo la juu la damu huchangia kuhisi maumivu hayo ya shingo na mgongo. Uchovu wa mwili kutokana na kazi za kila siku au msongo wa mawazo pia husababisha upate maumivu ya shingo na mgongo ambayo yanaweza kuwa makali sana au wastani.

Maumivu ya wastani huchukua muda mrefu na huendelea taratibu tofauti na yale makali ambayo huchukua muda mfupi lakini pia huweza kuchukua muda mrefu.


INAENDELEA. ….



Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.