Leo Mwenyezi Mungu ametuwezesha, zimetimia zaidi ya siku 42 toka mgonjwa wa mwisho kupona Marburg
Leo Mwenyezi Mungu ametuwezesha, zimetimia zaidi ya siku 42 toka mgonjwa wa mwisho kupona Marburg,
“Leo Mwenyezi Mungu ametuwezesha, zimetimia zaidi ya siku 42 toka mgonjwa wa mwisho kupona Marburg, Kwa maana hiyo tumekidhi vigezo vya Shirika la Afya Duniani vya kutangaza mwisho wa ugonjwa wa Marbung,
hivyo natangaza kwamba leo 02/06/2023 mlipuko wa ugonjwa wa Marburg tumeumaliza rasmi Mkoa wa Kagera.” @ummymwalimu
Waziri wa Afya Mhe. @ummymwalimu ameutarifu umma wa Watanzania na Ulimwengu kwa ujumla kuwa Tanzania imeweza kupambana na kudhibiti ugonjwa wa Marburg na hivi sasa kuwa Mkoa huo na nchi kwa ujumla ni salama na hakuna maambukizi ya ugonjwa huo.
Waziri Ummy amesema hayo leo kwenye kwenye kilele cha mapambano dhidi ya ugonjwa wa Marburg ambao uliripotiwa kuingia nchini mnamo Machi 16, 2023, Kagera Tanzania.