Mhe.Ummy Mwalimu:Ziara ya kikazi nchini India kufuatia Mwaliko wa Waziri wa Afya nchini India
Waziri wa Afya, Mhe. @ummymwalimu leo Julai 25, 2023 ameanza ziara ya kikazi nchini India kufuatia Mwaliko wa Waziri wa Afya na Ustawi wa Familia wa India Mhe. Mansukh Mandaviya.
Katika siku yake ya kwanza ya ziara yake nchini India, Mhe. Ummy amekutana na kufanya mazungumzo na mwenyeji wake Waziri Mandivya, Viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali ya kuimarisha ushirikiano katika Sekta ya Afya ikiwemo Huduma za Ubingwa Bobezi, upatikanaji wa Dawa zenye ubora na kwa bei nafuu, matumizi ya TEHAMA katika Huduma za Afya na udhibiti wa magonjwa yasiyoambukiza.
Katika ziara yake, Waziri Ummy ameongozana na watendaji ndani ya Sekta ya Afya wakiwemo, Mkurugenzi wa Huduma za Tiba kutoka Wizara ya Afya Prof. Pascal Rugajjo, Mfamasia Mkuu wa Serikali Bw. Daudi Msasi, Mkurugenzi wa Mamlaka wa Dawa na Vifaatiba TMDA Bw. Adam Fimbo pamoja na watumishi wengine ndani ya Sekta ya Afya.
via@wizara_afyatz