Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Ujio wa Cedric Kaze nao umechangia kwa sehemu kubwa timu kuchangamka zaidi

Aliyekuwa mshambuliaji wa Yanga SC, Fiston Mayele amefichua kuwa, aliekuwa Kocha wao Nasreddine Nabi pamoja na msaidizi wake, Cedric Kaze, walifungasha mabegi yao kabisa wakati wanakwenda kucheza mechi dhidi ya Club Africain.

Mayele ameyasema hayo kupitia documentary ya Yanga iliyozinduliwa hapo jana Agosti 7, 2023 ambapo mechi hiyo ya msimu uliopita wakati Yanga wakishiriki mashindano ya Shirikisho Afrika, ilikuwa imebeba hatma yao na endapo wangepoteza basi wangetolewa kwenye mashindano.

“Wakati tunaenda kucheza mechi ya marudiano dhidi ya Club Africain, Kocha Kaze alifungasha mabegi yake yote akamwambia mke wake tukirudi tunarudi Burundi.

“Kocha Nabi naye aliondoka na Mabegi yake yote halafu tukawa tunasikia kuwa kuna Kocha mpya,” Mayele akizungumza kwenye Documentary ya Yanga Sc.

KOCHA wa Yanga, Nasreddine Nabi amefichua kuwa, alitenga muda wa kutosha kuwafutilia Simba ndio maana alieleza jambo la kuwa na uhakika kwa kiasi kikubwa kupata ushindi katika mechi yao, lakini pia akasema ujio wa Cedric Kaze nao umechangia kwa sehemu kubwa timu kuchangamka zaidi.

Nabi alisema awali alikuwa anasikia taarifa kutoka katika maeneo mbalimbali wamepanga kumfukuza katika nafasi hiyo ndani ya siku saba zijazo pamoja na kupewa michezo miwili.

Alisema taarifa ambazo hazikuwa nzuri kwake jambo lililomuongezea umakini mkubwa yeye na wenzake kufanya maandalizi sahihi na wachezaji wake ili kuona wanachukua taji la kwanza.

 

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.