Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Rais aliyeondolewa madarakani nchini Niger Mohamed Bazoum kufunguliwa mashtaka kwa makosa ya uhaini

Rais aliyeondolewa madarakani nchini Niger Mohamed Bazoum kufunguliwa mashtaka kwa makosa ya uhaini

Viongozi wa mapinduzi nchini Niger wamesema jana usiku kuwa watamfungulia mashtaka Rais aliyeondolewa madarakani Mohamed Bazoum kwa makosa ya uhaini wa hali ya juu na kuzorotesha usalama nchini humo.

Utawala huo wa kijeshi umesema tayari umekusanya ushahidi utakaotumika kumshitaki Bazoum pamoja na Washirika wake wa ndani na wa nje kwenye vyombo vinavyoaminika vya kitaifa na kimataifa, hii ikiwa ni kwa mujibu wa taarifa iliyosomwa na Kanali Meja Amadou Abdramane kupitia Televisheni ya Taifa.

Bazoumu bado anazuiliwa kwenye Kasri la Rais, pamoja na Mtoto wake wa kiume na Mkewe tangu kulipofanyika mapinduzi hayo yapata wiki ya tatu sasa.

Taarifa hiyo ya kijeshi imesema Bazoum bado anaweza kuwasiliana na Watu wa nje kwakuwa hawajazuia mawasiliano kwenye Kasri hilo la Rais na bado anakutana na Daktari wake kila wakati na hata Jumamosi hii alikutana nae na taarifa ya Daktari huyo imesema Familia yote haikuwa na tatizo lolote la kiafya, hata hivyo Rais huyo amesema anashikiliwa mateka bila ya umeme na amekuwa akilishwa wali na tambi tu.

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.