Watu 10 wafariki kwenye ajali ya gari aina ya Toyota (Kirikuu) mkoani Kilimanjaro
Watu 10 wafariki kwenye ajali ya gari aina ya Toyota (Kirikuu) mkoani Kilimanjaro;
Watu 10 wamefariki dunia kufuatia ajali ya gari aina ya Toyota (Kirikuu) iliyogongana na gari la polisi Layland Ashok wakiwemo wafanyabiashara tisa (9) na askari polisi mmoja wa Chuo cha Polisi Moshi.
Mashuhuda wa tukio hilo wamesema chanzo cha ajali hiyo ni kupasuka tairi la kirikuu kisha kuhama barabara na ndipo magari hayo yalipokutana uso kwa uso.
Hospitali ya Kibong’oto imethibitisha kupokea miili ya watu 10 na miongoni mwao saba ni wanawake.