Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Madaktari Bingwa wa Moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete waifikia Kilimanjaro

Wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro na mikoa ya jirani wameishukuru Serikali kupitia Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kufikisha huduma za kibingwa za matibabu ya moyo mkoani Kilimanjaro.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa kambi maalum ya siku tano ya upimaji na matibabu ya moyo inayoendelea katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mawenzi (MRRH) wananchi hao wamesema uhitaji wa matibabu ya kibingwa ya magonjwa ya moyo mkoani humo ni mkubwa.

Elishadai Kimaro mkazi wa Kilimanjaro alisema kutokana na wingi wa watu kutoka mkoa wa Kilimanjaro na mikoa ya jirani idadi ya watu wanaohitaji matibabu ya moyo toka kambi hiyo kuanza imekuwa kubwa hivyo watu kurudishwa nyumbani na kurejea tena siku inayofuata.

“Ninaiomba Serikali huduma za matibabu ya moyo hapa mkoani kwetu zifanyike mara kwa mara au ikiwezekana tuwe na hospitali yetu inayotoa huduma hizi za matibabu ya moyo, kambi maalum ya siku tano na baadaye wataalamu kuondoka haitoshelezi kufikia mahitaji ya wanakilimanjaro”, alisema Kimaro.

Kimaro alisema kupitia kambi hiyo amepata nafasi ya kuchunguza afya ya moyo wake kwani alikuwa na hofu ya kuwa na matatizo ya moyo lakini hakujua ni nini afanye hadi hapo aliposikia ujio wa madaktari bingwa wa moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete hivyo naye kutumia fursa hiyo kupima.

Twaha Masawe mkazi wa Kilimanjaro alisema huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na wataalamu wa afya kutoka JKCI amezipenda kutokana na watoa huduma wanavyozungumza vizuri na wagonjwa na kuwapa elimu ya namna ya kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza.

Masawe alisema kupitia kambi hiyo ameelimishwa kutokuacha kutumia dawa za shinikizo la damu na kama ataacha anaweza kupata madhara katika moyo wake ama kupata kiharusi.

“Namshukuru Mungu toka nilipogundulika kuwa na shinikizo la damu nimekuwa nikitumia dawa, kupitia elimu niliyoipata hapa nitaendelea kutumia dawa kama inavyotakiwa sitapenda kuona napata madhara mengine ya kiafya yanayoletwa na tatizo la shinikizo la damu”, alisema Masawe

Forum Manager

Content creator&editor (Ms.Asifiwe)Jukumu langu kwako ni kuhakikisha unapata elimu ya kutosha pamoja na Updates mbali mbali ndani ya http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.