Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Wanajeshi 29 wa Niger wameuliwa kufuatia shambulio la kigaidi magharibi mwa nchi

Wanajeshi 29 wa Niger wameuliwa kufuatia shambulio la kigaidi magharibi mwa nchi, ikiwa ni idadi kubwa ya watu kuuliwa tangu wanajeshi kuchukua madaraka ya taifa hilo mwezi Julai.

Wizara ya ulinzi ilitangaza mauwaji hayo jumatatu usiku ikieleza kwamba kundi la wanajeshi wa usalama lilishambuliwa kaskazini magharibi mwa Tabatol, kwa kutumia mchanganyiko wa silaha ikiwa ni pamoja na vilipuzi na magari yaliyoendesha na karibu magaidi 100 walojitoa mhanga.

Wanajeshi wawili wamejeruhiwa vibaya na darzeni kadhaa ya magaidi waliuliwa.

Shambulio lilitokea karibu na mpaka wa Mali, wakati wa operesheni ya kijeshi iliyokua na lengo la kukabiliana na kuzia shambulio hilo lililofanywa na kundi la Islamic State katika eneo hilo kulingana na taarifa ya wizara.

Wizara ya ulinzi inasema mawasiliano kutoka magaidi walolazimika kukimbia yalinaswa, na kwamba washambuliaji walipata msaada kutoka waatalamu wa nje bila ya kutoa maelezo zaidi.

Taarifa imesema wanajeshi wamefariki kama mashuja na siku tatu za maombolezi ya kitaifa zimetangazwa.

Uwasi unaoendeshwa na wanamgambo wa kislamu umekumba kanda ya Sahel, magharibi ya Afrika kwa zaidi ya muongo mmoja, ukianzia kaskazini mwa Mali mwaka 2012 kabla ya kusamba katika nchi jirani za Niger na Burkina Faso mwaka 2015.

Mwezi Ogusti karibu wanajeshi 17 wa Niger waliuliwa na 20 kujeruhiwa katika shambulio linalodhaniwa lilifanywa na wanamgambo karibu na mpaka wa Niger na Burkina Faso.

Chanzo: Voa

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.