Hotel zakabiliana na mlipuko wa KUNGUNI Ufaransa
“Siku mbili zilizopita tuligundua kunguni na walikuwa tishio,” – mmiliki wa Hoteli ya Montlhery Paris Sud
Huwezi kujua kama wanasambaa kati ya chumba hadi chumba, na unaweza kushtakiwa ikiwa mgeni ataumwa vibaya, alisema.
Hoteli yake ni moja ya makampuni mengi yanayotafuta suluhu huku kukiwa na ongezeko la milipuko wa kunguni ulioripotiwa nchini Ufaransa na Uingereza.
Na makampuni sasa yanageukia teknolojia ya zamani na mpya ili kupata ufumbuzi na kuzuia kuenea zaidi.
Montlhery Paris Sud ililazimika kulipa kampuni ya kudhibiti wadudu zaidi ya dola 1,500 ili kukomesha wadudu hao kabla ya kuenea.
Je umewahi kukutana na wadudu hawa? ulitumia njia gani kutokomeza?