Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Tanzania na Zambia zinajipanga kuhakikisha Reli ya TAZARA inafanya kazi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali ya Tanzania na Zambia zinajipanga kuhakikisha Reli ya TAZARA inafanya kazi kwa uwezo wake wote na kuchochea uchumi wa nchi hizo mbili.

Akihutubia kwenye Bunge la Zambia jioni ya Oktoba 25, 2023, Rais Samia amesema kwasasa Reli hiyo inafanya kazi kwa asilimia nne tu ya uwezo wake jambo linalohitaji mabadiliko.

Reli ya TAZARA ina uwezo wa kusafirisha kiasi cha tani za mizigo Milioni Tano, lakini kwasasa kiasi cha tani 184,000 pekee, ndizo zinazosafirishwa.

Aidha, Rais Samia Suluhu Hassan (Tanzania) na Rais Hakainde Hichilema (Zambia), waliazimia kuweka mazingira yatakayofanya Biashara kati ya Mataifa haya mawili zisiwe na vikwazo.

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.