Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Mwimbaji Celine Dion hupata tiba ya physical therapy kila siku ili kupambana na ugonjwa wa stiff-person syndrome

Mwimbaji Celine Dion hupata tiba ya physical therapy kila siku, kupambana na ugonjwa usiotibika wa stiff-person syndrome.

Celine Dion anaripotiwa kupata ‘matibabu ya mwili yaani physical therapy kila siku’ huku akipambana na ugonjwa wa stiff-person syndrome, ugonjwa usio na tiba.

Mwimbaji huyo wa Kanada mwenye umri wa miaka 55, ambaye amepoteza udhibiti wa misuli yake kutokana na kuugua ugonjwa unaojulikana kama stiff-person syndrome, ugonjwa huu mpaka sasa hauna Tiba kamili,

kulingana na dada yake, Celine Dion anafanya kazi kwa bidii ili kuondokana na hali yake, kulingana na vyanzo mbali mbali vya habari.

‘Celine ni mpiganaji,’ mdadisi wa ndani aliambia  US Weekly. ‘Hana udhibiti mwingi juu ya misuli yake kama alivyokuwa hapo awali, lakini anafanya kazi na madaktari na wataalamu wa tiba ya mwili ili kupata nafuu.’

Chanzo hicho kilidai, ‘Celine amekuwa akichukua muda kuangazia afya yake lakini anapanga kupanda jukwaani tena mara tu atakapopewa idhini na timu yake ya matibabu.’

Mtu mwingine wa ndani pia aliongeza kuwa mwimbaji huyo ‘anaendelea kuimarika afya yake na amekuwa mwenye furaha zaidi na anamfanyia mazoezi ya mwili kila siku.’

‘Kurudi jukwaani kwa namna fulani ni ndoto yake ya mara kwa mara, hata kama hawezi tena kuimba; anataka tu kuona nyuso hizo zinazong’aa.’

Ugonjwa wa Stiff-person syndrome ni ‘ugonjwa nadra wa mfumo wa neva wa autoimmune ambao kwa kawaida husababisha kukakamaa kwa misuli na mikazo yenye uchungu ambayo huja na kuondoka na inaweza kuwa mbaya zaidi baada ya muda,’ kulingana na John Hopkins Medicine.

Mshindi huyo wa Grammy alionekana mara ya mwisho kwenye mchezo wa magongo huko Las Vegas akiwa na mapacha wake Eddy na Nelson, wenye umri wa miaka 13, na mwanawe mkubwa Charles-Rene, mwenye umri wa miaka 22, wakitazama Montreal Canadiens.

Celine Dion alisema;

“My boys and I had such a fun time visiting with the Montreal Canadiens after their hockey game with Vegas Golden Knights in Las Vegas Monday night,’ the My Heart Will Go On singer posted November 1.

‘They played so well, what a game!! Thank you for meeting us after the game, guys! That was memorable for all of us. Have a great season! – Celine xx”… ‘

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.