KUSHINDWA KUDHIBITI SUKARI NA KUONGEZEKA KWA MAJI YA UZAZI
KUSHINDWA KUDHIBITI SUKARI NA KUONGEZEKA KWA MAJI YA UZAZI
Kwa wanawake wenye kisukari, kushindwa kudhibiti kiwango cha sukari kwenye damu wakati wa ujauzito huweza kuleta madhara mbali mbali.
kushindwa kudhibiti kiwango cha sukari kwenye damu wakati wa ujauzito huweza Kupelekea kuongezeka kwa kiwango cha sukari kwenye damu ya mtoto aliyetumboni,
hali ambayo huweza kusababisha kuongezeka kwa kiwango cha mkojo kutoka kwa mtoto na hivyo kuongezeka kwa maji maji ya uzazi au amniotic fluid.
Lakini pia sukari kwa mama mjamzito inahusishwa na kuathiri utengenezwaji wa viungo mbalimbali kwa mtoto aliyetumboni,
na yote haya yanaweza kupelekea changamoto mbalimbali ambazo miongoni mwake ni kuongezeka kwa maji ya uzazi au kwa kitaalam amniotic fluid.
Kiwango kikubwa cha maji haya ya uzazi yanayosaidia mtoto kuelea awapo katika mji wa mimba huweza kusababisha madhara mengine,
Maji ya uzazi yakizidi kuliko inavyotakiwa huweza kusababisha;
– kuzaa kabla ya wakati,
– Chupa ya uzazi au tando kupasuka kabla ya wakati,
– mlalo usio sahihi wa mtoto aliyetumboni n.k
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.