Faida za Vijana kupata Elimu ya Afya na uzazi
Faida za Vijana kupata Elimu ya Afya na uzazi
• • • • •
FAIDA ZA UTOAJI WA ELIMU YA AFYA NA UZAZI KWA VIJANA
Kuna umuhimu mkubwa kwa vijana kupata elimu ya afya na uzazi hata wakiwa mashuleni.
Huu sio wakati wa kuona aibu kuzungumzia maswala ya afya ya uzazi na kutoa Elimu kwa Vijana wetu,
FAIDA ZA UTOAJI WA ELIMU YA AFYA NA UZAZI KWA VIJANA NI PAMOJA NA;
– Kusaidia vijana kutambua mabadiliko makubwa ambayo hutokea katika miili yao kipindi cha ukuaji wao
– Kusaidia kupunguza au kuondoa kabsa tatizo la mimba katika umri mdogo
– Kusaidia kupunguza kwa kiwango kikubwa maambukizi ya magonjwa mbali mbali ya Zinaa kama Kisonono,kaswende,chlamydia(pangusa) pamoja na Ugonjwa wa UKIMWI
– Kujikinga na magonjwa mbali mbali kama vile UTI,FANGASI Sehemu za Siri, PID n.k
– Kujenga uelewa mpana kuhusu afya pamoja na Jinsi ya kujilinda na magonjwa,
KUMBUKA; Asilimia kubwa ya magonjwa yasio yakuambukiza kama vile; Kisukari,Presha,magonjwa ya moyo n.k hutokana na mtindo mbaya wa maisha ikiwemo ulaji wetu wa kila siku.
vyakula gani ule na vyakula gani usipendelee kula kila siku
Hivo kuna umuhimu mkubwa wa watu kupata elimu ya kutosha kuhusu Ulaji wa Kila siku, Pamoja na mtindo wa maisha kwa ujumla,
Kujua Umuhimu wa Kufanya Mazoezi ya mwili
– Kusaidia kujenga jamii yenye afya bora pamoja na nguvu N.K