Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

Dalili za Mtu kuwa na Allergy dhidi ya Vitu mbali mbali

Dalili za Mtu kuwa na Allergy dhidi ya Vitu mbali mbali,

Hizi hapa ni baadhi ya dalili ambazo huweza kukuonyesha kwamba una shida ya Mzio au allergies kwenye baadhi ya Vitu.

1. Kuvimba Pua muda mfupi baada ya kutoka nje, hii ni allergic rhinitis, ambapo mtu hupata reaction dhidi ya particles ndogo kwenye hewa anayovuta.

Kuvimba pua baada ya kukaa sehemu zenye vumbi,kula chakula flani,dawa n.k

2. Mtu kupiga chafya sana hata baada ya kula kitu chochote,

3. Kuwashwa Sana Mwilini, na wakati mwingine kupata vipele kwenye ngozi

4.macho kutoa machozi yenyewe, na baadhi ya watu hupata shida hii baada ya kuanza kunywa dawa ambazo hawajawahi kuzitumia kabsa.

5. Mtu kuvimba Mdomo baada ya kula baadhi ya vyakula

6. Mtu kuwashwa sana masikio au Mdomo, hasa baada ya kula chakula flani

7. Mtu kuvimba mdomo,uso,pua n.k baada ya kuoga kwa kutumia baadhi ya sabuni

8. Kupata shida ya kupumua,kila unapokula nyama au chakula flani

9.Ngozi kubadilika rangi,kuwasha,kuwa na vipele,baada ya kula baadhi ya vyakula,dawa n.k

10. Kupata kichefuchefu,kutapika,maumivu ya tumbo au Kuharisha,kila unavyokula baadhi ya vyakula

11. Mtu kuvimba Ulimi au Lips za mdomo baada ya kula baadhi ya vyakula,Dawa n.k

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.