Dalili za Mtu kuwa na Allergy dhidi ya Vitu mbali mbali
Dalili za Mtu kuwa na Allergy dhidi ya Vitu mbali mbali,
Hizi hapa ni baadhi ya dalili ambazo huweza kukuonyesha kwamba una shida ya Mzio au allergies kwenye baadhi ya Vitu.
1. Kuvimba Pua muda mfupi baada ya kutoka nje, hii ni allergic rhinitis, ambapo mtu hupata reaction dhidi ya particles ndogo kwenye hewa anayovuta.
Kuvimba pua baada ya kukaa sehemu zenye vumbi,kula chakula flani,dawa n.k
2. Mtu kupiga chafya sana hata baada ya kula kitu chochote,
3. Kuwashwa Sana Mwilini, na wakati mwingine kupata vipele kwenye ngozi
4.macho kutoa machozi yenyewe, na baadhi ya watu hupata shida hii baada ya kuanza kunywa dawa ambazo hawajawahi kuzitumia kabsa.
5. Mtu kuvimba Mdomo baada ya kula baadhi ya vyakula
6. Mtu kuwashwa sana masikio au Mdomo, hasa baada ya kula chakula flani
7. Mtu kuvimba mdomo,uso,pua n.k baada ya kuoga kwa kutumia baadhi ya sabuni
8. Kupata shida ya kupumua,kila unapokula nyama au chakula flani
9.Ngozi kubadilika rangi,kuwasha,kuwa na vipele,baada ya kula baadhi ya vyakula,dawa n.k
10. Kupata kichefuchefu,kutapika,maumivu ya tumbo au Kuharisha,kila unavyokula baadhi ya vyakula
11. Mtu kuvimba Ulimi au Lips za mdomo baada ya kula baadhi ya vyakula,Dawa n.k
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.