Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

MADHARA YA KUTUMIA EARPHONES MASIKIONI

YAJUE MADHARA YA KUTUMIA EARPHONES MASIKIONI

Sauti kutokana na matumizi mabaya ya spika za masikioni (earphones & headphones) zaweza kutuweka katika hatari ya kupata uziwi. Katika zama hizi za maendeleo ya digitali, kumekuwepo ongezeko la matumizi la vifaa vya kielektroniki kama rununu, runinga na kompyuta. Matumizi ya vifaa hivi huambatana na spika za mezani pamoja na spika za masikioni ili kumraisishia mtumiaji kusikiliza na kufurahia muziki. Spika za masikioni zimetengenezwa ili kumuwezesha mtumiaji kusikiliza sauti kutoka katika kifaa chake wakati wowote atakapohitaji na hata kama amezungukwa na mazingira yenye kelele.

Usikilizaji wa sauti ya juu au sauti kubwa kwa kutumia spika za masikioni kwa muda mrefu kunaweza kupelekea kupata uziwi pia hata uziwi wa moja kwa moja. Usikilizaji huu wa sauti kubwa ni hatari zaidi kwa watoto na vijana kwa kuwa hupendelea kusikiliza muziki kwa sauti ya juu aidha nyumbani au katika vilabu vya muziki, kwenye magari na hata kwa kutumia spika za masikioni.

Sauti hupimwa kwa kutumia skeli ijulikanayo kama decibel (dB).Mfano mtu anayeongea kwa sauti ya chini ni kadirio la 30 dB.

Kwa mujibu wa shirika la afya duniani (WHO), kupitia takwimu zilizopatikana katika nchi zenye kipato cha kati zinaonyesha kuwa, miongoni mwa wale walio na umri kati ya miaka 13-35,karibu asilimia 50 husikiliza sauti katika kiwango kisicho salama kwa kutumia vifaa vyao binafsi vya sauti na asilimia 40 huwa katika kiwango kisicho salama cha sauti wakiwa katika kumbi za starehe

Shirika la afya (WHO) limeainisha kuwa, kukaa eneo lenye kiwango cha sauti kuanzia 85dB kwa masaa nane au 100dB kwa dakika 15 kuwa siyo salama. Inakadiriwa kuwa 1.1bilioni ya walio chini ya miaka ishirini(teenagers) na vijana wako katika hatari ya kupoteza usikivu kutokana na matumizi ya vifaa vya hivi zikiwemo simu za mkononi(smartphones) zinazoambatana na spika za masikioni.

Inashauriwa kuwa kiwango cha juu cha sauti katika maeneo ya kazi ni 85dB na isizidi masaa nane kwa siku. Wafanyakazi wa vilabu vya usiku na baa mara nyingi huwa katika kiwango cha juu cha sauti na wanashauriwa kupunguza masaa ya kazi. Kwa mfano katika klabu za usiku, huwa na kiwango cha 100dB kwa hiyo itakuwa salama kwa masikio yetu tukipunguza muda.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!

 

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.