CHUNUSI USONI NI NINI? NA HULETWA NA NINI?
CHUNUSI
• • • • • •
Chunusi ni nini?
Chunusi ni ugonjwa wa ngozi unaowaathiri watu wengi katika kipindi fulani cha maisha yao. Ugonjwa huu husababisha vipele vidogo vidogo vya mafuta kwenye ngozi na wakati mwingine hufanya ngozi kuwa na maumivu au kuhisi kuungua. Viupele hivi hutokea wakati vishimo vya kupitisha jasho katika ngozi vinapozibwa kwa mafuta na seli za ngozi zilizokufa au wadudu yaani bakteria. Mara nyingi chunusi hutokea usoni, mgongoni, kifuani na shingoni. Chunusi huwaathiri takribani asilimia 80% ya watu.
Wanawake wengi wamekua wakihangaika na matatizo mbalimbali ya ngozi,kama vile;
➡Chunusi sugu usoni na mgongoni
➡Mabaka,makovu upele na harara
➡ngozi kuwa kavu na inayotoa jasho sana
➡ngozi iliyoungua kutokana na matumizi ya vipodozi
➡Kukosa unyevu katika ngozi
➡Madoa meusi yasiyoisha(black heads)
➡Makunyanzi na ngozi iliyozeeka
Kwa kawaida ngozi ya mwanamke tofauti na mwanaume,inatakiwa kuwa laini, nyororo na isiyo na madoa wala ukavu…hii ni kutokana na uwepo wa hormone ya oestrogen inayozalisha vichocheo kwa ajili ya ngozi nzuri
Tatizo la ngozi hutokea pale tunapokutana na changamoto za kawaida katika maisha ya kila siku kama vile vyakula,matumizi ya vipodozi na mtindo wa maisha kwa ujumla…tatizo huwa haliishi kwa sababu hutibiwa nje tuu sehemu inayoonekana,na sio chanzo cha tatizo yaani ndani
Kw ushauri zaidi,elimu au Tiba tuwasiliane kwa namba +255758286584.