Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

DALILI ZA OVARIAN CYSTS(VIUVIMBE KWENYE MIFUKO YA MAYAI)

OVARIAN CYSTS

• • • • • •

Dalili Za Ovarian Cysts

 

Ovarian cysts nyingi hazitambuliwi na hupotea zenyewe bila hata mwanamke mwenyewe kujua kuwa alikuwa nazo. Wakati cysts zinaonyesha dalili, maumivu maeneo ya tumbo au kwenye nyonga hujitokeza. Maumivu haya husababishwa na:


. kupasuka kwa cyst,

. ukuaji wa haraka na kunyumbuka,

. damu kutoka kwenye cyst,

. kujinyonga kwa cyst kwenye mishipa ya damu (torsion).


Kama cyst imekuwa kubwa, dalili nyingine huweza kujitokeza kutokana na msukumo au kujinyonga kwa viungo vingine vya mwili vilivyo karibu (torsion). Endapo ovari itajinyonga au kuhama kutoka sehemu yake ya awali, mtiririko wa damu kuelekea kwenye ovari hukatwa, na kama hakuna tiba itakayotolewa, tishu za ovari zinaweza kuharibika au kufa. Ovarian torsion inachangia asilimia 3 ya upasuaji wa dharura wa viungo vya uzazi vya akina mama. Katika mazingira hayo dalili hizi zinaweza kujitokeza:


. kujaa kwa tumbo, kutanuka tumbo,

. maumivu eneo la chini ya mgongo,

. chakula kutomeng’enywa tumboni,

. kusikia umeshiba baada ya kula chakula kidogo tu

. kusikia haja ndogo kwa ghafla

. kushindwa kumaliza kabisa haja ndogo

. Kujisikia haja kubwa kila wakati

. kupata haja kubwa kwa shida

. maumivu wakati wa tendo la ndoa



Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.