FAHAMU JINSI YA KUONGEZA DAMU KWA KUTUMIA VYAKULA KAMA PILIPILI HOHO
DAMU
• • • • • •
Soma hapa kama unataka kupandisha damu yako haraka wakati wa ujauzito na kwa wasio wajawazito pia..!
Katika nchi zenye kipato kidogo tunategemea kupata madini ya chuma kutoka katika mboga za majani na vyakula vingine vyenye asili ya mimea kama maharage, Spinach na juisi pendwa ya maji ya matembele.. hata hivyo mwili unaweza kupata asilimia 10 ya madini ya chuma kutoka kwenye vyakula hivyo ukilinganisha na asilimia 30 kutoka kwenye nyama na samaki.
Kwa hiyo ni muhimu kula vyakula vingine vyenye Vitamin C ili kusaidia kuchukuliwa kwa madini ya chuma kwa urahisi kutoka katika vyakula hivyo. Vyakula hivi vifuatavyo vina kiwango kikubwa cha Vitamin C, ukivitumia pamoja na vyakula vyenye madini ya chuma vitapandisha damu yako haraka..
▫️Broccoli ?
▫️Pilipili Hoho
▫️Nyanya na tomato sauce ?
▫️Zabibu na juisi ya Zabibu ?
▫️Machungwa na juisi ya Machungwa ?
▫️Strawberry ?
▫️Kiwi ? (sio kiwi ya kung’arisha viatu kuna tunda linaita kiwi)
Ili kujua vyakula vyenye madini ya chuma kwa ajili ya kuongeza damu,endelea kutufwatilia