HATUA AMBAZO MWANAMKE HUPITIA KATIKA UKUAJI WAKE AMBAZO ASIPOZINGATIA BAADHI YA MAMBO AFYA YAKE HUWA KATIKA HATARI
MWANAMKE
• • • • • •
Katika ukuaji wa mwanamke zipo hatua ambazo huzipitia na hatua hizo huweza kumpelekea KUPATA matatizo ha kiafya endapo hatozingatia Mambo muhimu ya kiafya.
Hatua hizo ni kama
● kupevuka na kuanza Hedhi
● kukutana kimwili na Mwanaume
● Kubeba ujauzito na kujifungua
● Kufikia Ukomo wa Hedhi.
Hivyo vyote ni vitu vinavyoujenga lakini pia kuathiri Mwili wa mwanamke kwa sehmu kubwa.
Wanawake wengi hujikuta katika changamoto za kiafya kutokana na maambukizi ,kupoteza madini muhimu na mengine yanatokana na mabadiliko ya mwili kutokana na umri, mtindo wa maisha au urithi katika vina saba.
Changamoto hizo ni pamoja na
■ Fungus /Fungus Sugu
■ UTI /UTI sugu
■ PID (Vimbe katika Via vya UZAZI)
■ Hormones Imbalance
■ CYCTS (Vimbe kama maji maji katika mayai)
■ Fibroids (Vimbe kwneye kizazi)
Nk
Changamoto hizi hua na dalili mbali mbali na baadhi ya dalili hufanana
Mfano
● Miwasho, Uchafu, harufu mbaya
● Maumivu makali wakati wa Hedhi
● Kutokwa Damu nyingi wakati wa Hedhi na wakati mwingine damu yenye uchafu au mabonge
● Kupungukiwa damu mara kwa mara.
● Maumivu wakati wa tendo la ndoa
● Maumivu Kwenye tumbo chini ya kitovu au pembeni
● Kutokupata Ute Wa UZAZI siku za hatari au ukavu uliopitiliza.
● Kutokushika ujauzito au ujauzito kuharibika
● Maumivu makali ya kichwa haswa kipanda Uso.
● Maumivu ya mgongo, kiuno na nyonga.
Nk.
Watu wengi hutibu Dalili hizo na sio chanzo cha tatizo, hivyo kupelekea hali hizo kuondoka kwa muda Na kisha kurejea na kusababisha hali kuwa mbaya zaidi.