Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

IJUE ZAO LA MCHAICHAI NA FAIDA ZAKE LUKUKI

MICHAICHAI

• • • • • •

IJUE ZAO LA MCHAICHAI NA FAIDA ZAKE LUKUKI.

Mchaichai ni aina ya majani upandwao kwa ajili ya mahitaji ya binadamu, asilimia kubwa huotesha pembezoni mwa nyumba zao kwa kusudi la kutumiwa kama kiungo cha chai, kinachojulikana kwa jina la lemongrass kwa lugha ya kiingereza na cymbopogon kwa lugha za wataalam  wa mimea, ilianza kulimwa  nchini uphilipino mnamo Karne ya 17 baadae ukaingia katika nchi ya Haiti mwaka 1799  ambapo kilimo kilishamiri hadi mwaka 1917 wataalam wa mimea wakaanzisha mashamba ya mchaichai kwa ajili ya utafiti Nchini marekani, miaka ya 1947 soko la mchaichai ukarasimishwa katika jimbo la calfonia.

Mataifa mengine kama India, Sri lanka, Argentina, Australia na kusini mwa Amerika kwa asilimia kubwa walitilia maanani zao hilo hadi kufikia mwaka 1905 wataalam wa mimea kutoka  sehemu mbalimbali ulimwenguni walifanikiwa kuibua faida lukuki za mchaichai na kupelekea kuenea dunia nzima.

FAIDA ZA MCHACHAI KIAFYA.

Wataalamu wa mimea na lishe  walithibitisha uwezo wa mchaichai kuwa inasaidia kutibu na kudhibiti magonjwa kama  maumivu ya tumbo,maambukizi katika njia ya mkojo (U.T.I), inasaidia kusafisha figo na ini, matatizo ya moyo( Bp), inaimarisha utendaji kazi ya mishipa ya fahamu,inasaidia kudhibiti mlundikano wa mafuta katika mishipa ya damu (lehemu), inaondoa  sumu mwilini, inaongeza kinga za mwili(CD4), inatibu Saratani, Inatibu kisukari aina ya pili,inatibu Baridi yabisi, Inaimarisha afya ya ngozi,inasaidia tatizo la kukosa usingizi (insomnia ), inatibu maumivu ya tumbo la hedhi, inatoa gesi tumboni, inatibu homa za Mara kwa Mara, kutapika na maumivu ya viungo.

Wataalamu wa lishe na tiba kwa kutumia mimea na matunda, walibainisha kuwa uwezo huo ni kutokana na kwamba zao la mchaichai umesheheni virutubisho na misombo mbalimbali ambayo ni muhimu sana kwa afya ya binadamu kama vile;

Vitamin A,B1 (thiamine ),B2(Riboflavin ),B3 (niacin ),B5 (pantothenic acid ),B6 (pyridoxine),folate na vitamin C pamoja na madini ya potassium, madini Chokaa, magnesium, manganese, Copper, zinc na  phosphorus.

Mbali na virutubisho tajwa mchaichai ni zao pekee ambalo viambata tiba vinapatikana kwa kiasi kikubwa, ndio maana dunia inatizama kwa jicho la

tatu, kutokana na kemikali tiba kama

luteoil,glycosades,quercetin,Kaempferol, elimicin,catecol, chlororogenic acid, citral na Caffeic acid.

Viambata tiba hivyo vinasaidia kudhibiti magonjwa hatarishi kama kupooza, aina mbalimbali za Saratani,vivimbe mwilini, matatizo ya mifupa na magonjwa sugu.

HUTIBU SHINIKIZO LA JUU LA DAMU NA UNENE KUPITA KIASI.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na chuo kikuu cha wisconsin mwaka 1989, mchaichai una virutubisho vya madini ya potassium pamoja na misombo (compounds) za lemonal, citral na quercetin .

Aidha, utafiti uliofanyika December 2009 na kuchapishwa katka jarida la The Indian Journal of biochemistry and biophysics ulidhibitisha uwepo wa madini ya potassium, magnesium na misombo aina ya flavonoids katika mchaichai.

Wataalamu mbalimbali wanabainisha kuwa, virutubisho hivyo vinavyopatikana katika mchaichai vina uwezo mkubwa wa kuondoa mlundikano wa mafuta mwilini ambayo husababisha unene wa kupitiliza.

Pia huondoa mlundikano wa mafuta katika mishipa ya damu, hivyo kuiruhusu damu kupita vizuri katika sehemu mbalimbali za miwili.

Kuondolewa kwa mafuta hayo katika mishapi ya damu hushusha shinikizo la  juu  la damu na kufanya mapigo ya moyo kuwa katika hali ya kawaida.

Sambamba na kudhibitiwa mlundikano wa lehemu katika mishipa ya damu hasa ateri, huifanya mishipa hiyo kuwa na afya njema, pia na kinga dhidi ya ugonjwa wa kiharusi.

JINSI YA KUTUMIA.

Kupata tiba hiyo, majani ya mchaichai yalowekwe katika maji ya moto kiasi cha vikombe vitatu vya chai, weka majani manne hadi sita mgonjwa  anywe maji hayo kiasi cha kikombe kimoja  cha chai kabla ya kula chochote asubuhi, mchana, nusu saa kabla ya mlo, na jioni kabla ya chakula cha jioni.

Mgonjwa anaweza kutia sukari kwa kiasi kidogo mno. Tafiti zinabainisha kuwa mtu mwenye Matatizo ya shinikizo la juu la damu  akitumia  tiba hii kwa muda wa miezi  miwili  atakuwa ameshaondokana na tatizo husika.

TIBA YA KISUKARI.

Wataalamu wa tiba kwa kutumia mimea na lishe walibainisha kuwa katika zao la mchaichai una kirutubisho kinachofahamika kwa jina la citral.Tafiti mbalimbali zinaelekeza kuwa,kirutubisho hicho huweka sawa kiwango cha insulini mwilini.Hivyo kwa Wagonjwa wa Kisukari ambao kiwango chao cha insulini ni kidogo,wanapotumia mchaichai wanapata faida kubwa kuudhibiti ugonjwa wa kisukari .

Ifahamike kuwa,insulini ni kichocheo (hormone) kinachotokewa na tezi ya kongosho ambacho kina kazi ya kuweka sawa kiwango cha sukari mwilini. Wapo insulini itakuwa ndogo sana basi sukari itaongezeka na kusababisha athari mbaya katika mifumo mbalimbali ya mwili.

JINSI YA KUTUMIA.

Kupata tiba hiyo,majani ya mchaichai huchemshwa katika maji kisha maji hayo kiasi cha kikombe kimoja cha chai yatiwe unga wa tangawizi kiasi cha vijiko 2 vidogo. Mgonjwa anywe maji hayo kiasi cha kikombe 1 asubuhi kabla kula kitu chochote na jioni kabla ya chakula cha usiku .Tiba hii itumike kila kwa muda wa mwezi mmoja.

HUTIBU VIDONDA VYA TUMBO.

Chanzo kikuu cha vidonda vya tumbo ni bacteria wanaofahamika kama Helicobacter pylori .Wataalamu wa lishe wanabainisha kuwa,kirutubisho cha citral kinachopatikana katika mchaichai kina uwezo mkubwa wa kuidhibiti bakteria hao hatari na hivyo  kutibu ugonjwa wa vidonda vya tumbo.

JINSI YA KUTUMIA.

Chemsha majani  kumi za  mchaichai  Kwa maji kiasi cha nusu lita,mgonnjwa anywe maji hayo kiasi cha kikombe kimoja asubuhi na usiku kabla ya kulala.

Tatizo la maumivu makali wakati wa hedhi na kuvurugika kwa mzunguko.

Wataalamu wa tiba kwa kutumia mimea tiba na lishe Walibaini kuwa,kunywa chai iliyotengenezwa kwa  kuchanganywa mchaichai na tangawizi ni tiba kwa tatizo ya tatizo la maumivu  makali ya tumbo yanayosababishwa na hedhi pamoja na kurekebisha mzunguko wa hedhi uliovurugika.

JINSI YA KUTUMIA.

Kupata tiba hiyo,majani ya mchaichai huchemshwa katika maji,kisha maji hayo kiasi kikombe  cha chai yatiwe unga wa tangawizi kiasi cha vijiko viwili vidogo,kisha mgonjwa anatakiwa kunywa mchanganyiko huo vijiko vinne vikubwa Mara nne kwa siku kila baada ya masaa matatu ndani ya siku saba hadi kumi na nne.

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.