Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

MTOTO KUZALIWA NA MABAKA MABAKA MAKALIONI NA MGONGONI(mongolian spot)

 MONGOLIAN SPOT

• • • • •

MTOTO KUZALIWA NA MABAKA MABAKA MAKALIONI NA MGONGONI(mongolian spot)


Mtoto huweza kuzaliwa akiwa na mabaka mabaka ya rangi ya blue hasa hasa maeneo ya makalioni na mgongoni, mabaka mabaka haya kwa kitaalam hujulikana kama Mongolian spot.


MABAKA MABAKA HAYA HUDUMU KWA MUDA GANI?


Mabaka mabaka(mongolian spot) huweza kupotea yenyewe ndani ya muda mfupi au kudumu  kwa kipindi kirefu hata miaka Minne na kuendelea, 


Kwa wengine hupotea yenyewe baada ya mtoto kufikia umri wa kubalehe Na baadhi ya watoto wachache mabaka mabaka haya huendelea kuwepo maisha yao yote.


CHANZO CHA MABAKA MABAKA HAYA NI NINI?


– Chanzo cha mabaka mabaka haya au Mongolian spot, ni kutokana na uwepo mkubwa wa seli hai kwa ajili ya kuleta rangi kwenye ngozi maarufu kama melanocytes hasa hasa maeneo ya makalioni na mgongoni, 


ndyo sababu kubwa ya rangi ya ngozi katika maeneo haya kubadilika na kuwa blue kutokana na uwepo wa kiwango kikubwa cha Melanocytes ambazo huzalisha melanin(kwa ajli ya kuipa ngozi rangi yake).


MATIBABU YA MONGOLIAN SPOT


– Tatizo hili kwa mtoto huweza kuisha lenyewe wala hakuna matibabu yoyote ambayo hufanyika kwa mtoto mwenye shida hii kwenye ngozi yake


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE LA KIAFYA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.