KUWA MWENYE AFYA KABLA NA WAKATI WA UJAUZITO KWA KUFANYA HAYA
KUWA MWENYE AFYA KABLA NA WAKATI WA UJAUZITO KWA KUFANYA HAYA
Zingatia mambo haya kabla na wakati wa ujauzito ili kumkinga mtoto aliyetumboni kupata shida yoyote yaani Birth defects.
• Hakikisha unapata mlo kamili yaani Balance Diet,
Mlo wenye virutubisho vyote kwa kiwango kinachohitajika mwilini
• Kuzingatia matumizi sahihi ya Folic acid au FEFOL,
Vidonge vyekundu vya kuongeza damu,kuzuia matatizo kama vichwa vikubwa,mgongo wazi n.k
• Hakikisha unahudhuria kliniki zote yaani antenatal Care visits
• Fanya vipimo muhim kama vile Ultrasound, kipimo cha malaria,Group la damu,wingi wa damu,presha,uwepo wa protein kwenye mkojo,kaswende(syphilis) n.k
• Fanya mazoezi mbali mbali ya mwili mara kwa mara
• Epuka matumizi ya Pombe na Sigara ukiwa mjamzito
• Epuka matumizi ya dawa hovio pasipo maelekezo kutoka kwa wataalam wa afya
• Jikinge na magonjwa yote ya zinaa kama vile kaswende/syphilis pamoja na magonjwa mengine kama vile ZIKA,RUBELLA n.k
KUMBUKA: Afya Bora kabla ya ujauzito na kipindi cha ujauzito,ndyo matokeo chanya ya afya kwa Mtoto atakayezaliwa.
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.