Kuwa Mlemavu haimaanishi huwezi kila kitu,unaweza kutimiza ndoto zako
Kuwa Mlemavu haimaanishi huwezi kila kitu,unaweza kutimiza ndoto zako,
Jamii nyingi zimekuwa na dhana potofu na kuwaona walemavu hawawezi chochote,
ila ukweli ni kwamba,Hata kama ni mlemavu ana uwezo wa kufanya kitu kikubwa,
Mpe nafasi, usimfiche,usimnyanyapae, mpe haki yake ya elimu, msaidie kutimiza malengo yake.
Na Tafiti zinaonyesha, Walemavu wanakuwa na uwezo mkubwa sana wa kufanya vitu vikubwa hata kuliko ambao wapo sawa,
Wakipewa nafasi hutimiza ndoto zao na kufanya mambo makubwa na kwa uwezo mkubwa duniani kote.
Mungu huwapa Nguvu ya tofauti sana ya kufanya mambo yao kuliko mtu mwingine yoyote.
Tusaidie kuelimisha jamii yako, Kuwa mlemavu haimaanishi huwezi kila kitu, Wape nafasi ya kuonyesha uwezo wao na kutimiza ndoto zao.
#WatuwoteniSawa #jamii