Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

Mtoto anaanza kukaa miezi mingapi? soma hapa kufahamu

Mtoto anaanza kukaa miezi mingapi? soma hapa kufahamu

HATUA ZA UKUAJI WA MTOTO BAADA YA KUZALIWA

Zifahamu hatua mbali mbali za ukuaji kwa mtoto(Stages of development) au kwa kitaalam zaidi hujulikana kama Developmental milestones, Hatua hizi za ukuaji zinahusisha mtoto mwenye afya bora ambaye hana tatizo lolote ambalo linaweza kuchelewesha ukuaji wake.

Fahamu kwamba matatizo kama vile; Utapiamlo, upungufu wa baadhi ya vichocheo au hormones mwilini, matatizo ya Ubongo,mtoto kukosa hewa ya kutosha ya oxygen kwenye ubongo n.k vyote hivi huweza kuchelewesha ukuaji na maendeleo ya mtoto wako

Tangia mtoto anazaliwa mpaka anakuwa mtu mzima kuna hatua mbali mbali za ukuaji ambazo anazipitia huku zikihusisha mambo mbali mbali kama vile mabadiliko ya mwili,tabia n.k

HATUA ZA UKUAJI WA MTOTO BAADA YA KUZALIWA

1. MARA TU BAADA YA MTOTO KUZALIWA
Mara tu baada ya mtoto kuzaliwa huanza kupata mabadiliko mbali mbali kwenye mwili wake, ndani ya siku 7-10 baada ya mtoto kuzaliwa huanza kupungua uzito wake wa mwili kwa asilimia 5% mpaka 10%,
Baadae mtoto huanza kuongezeka uzito wake wa mwili tena, Watoto wengi huzaliwa na urefu wa sentimita 50, baada ya mwaka mmoja hufikisha sentimita 75 na baada ya miaka minne hufikisha urefu wa sentimita 100.

Kwa kawaida mtoto huzaliwa na kichwa chenye mzunguko  wa sentimita 35 na kuongezeka sentimita moja kila mwezi na baada ya miezi 12 kichwa hufikisha sentimita 46

2. WIKI YA SITA BAADA YA MTOTO KUZALIWA

Katika kipindi hiki au umri huu mtoto huendelea kupata mabadiliko mbali mbali mwilini ikiwa ni pamoja na kutabasamu pasipo kuongea kitu chochote.

3. MWEZI WA PILI BAADA YA MTOTO KUZALIWA

Kwenye mwezi wa pili, mtoto huanza kukunja na kunyoosha mikono huku akivuta nguo zake na za mtu mwingine aliyembeba.

4. MWEZI WA NNE BAADA YA MTOTO KUZALIWA

Mtoto anapofikisha umri wa miezi minne huanza kushika vitu na kuviweka mdomoni na kuanza kugeuka pale anaposikia sauti ya mtu inaita na kuweza kutumia shingo yake vizuri zaidi.

5. MWEZI WA SITA BAADA YA MTOTO KUZALIWA

Katika kipindi hiki mtoto huendelea kupata mabadiliko mbali mbali mwilini ikiwa ni pamoja na kuanza kuota meno, kuanza kutambaa, kuanza kukaa mwenyewe na kupata wasiwasi akimuona mtu ambaye hamfahamu.

6. MWEZI WA TISA BAADA YA MTOTO KUZALIWA

Kwenye mwezi wa tisa; mtoto huanza kusimama mwenyewe na kuanza kuita majina mbali mbali kama vile mama,baba,dada, kaka na kuanza kucheza michezo ya kitoto.

7. MWEZI WA 12 BAADA YA MTOTO KUZALIWA

Baada ya mtoto kufikisha umri wa mwaka mmoja toka azaliwe yaani miezi 12, ndipo huanza kutembea mwenyewe kwa kukusaidiwa na vitu mbali mbali baada ya kuvishika au kwa  kushikwa na mtu japo baadhi ya watoto wengine huwahi zaidi kuanza kutembea hata kabla ya mwaka kuisha.

8. MWEZI WA 15 BAADA YA MTOTO KUZALIWA

Mwezi wa 15 mabadiliko mbali mbali huendelea kutokea ikiwa ni pamoja na uwezo wa mtoto kutembea mwenyewe, Mtoto kuweza kuchora mstari na kuonyesha kitu anachokihitaji kwa kidole pamoja na vitu vingine.

9. MWEZI WA 18 BAADA YA MTOTO KUZALIWA

Hapa mtoto huweza kupanda ngazi, huongeza idadi ya maneno na hufuata akiagizwa kufanya au kutofanya kitu fulani, hapa huanza kutumia kijiko na kujishika sehemu za mwili wake.

10. MIAKA MIWILI(2) BAADA YA MTOTO KUZALIWA

Mtoto anapofikisha umri wa miaka miwili, huweza kufanya vitu vingi zaidi kama vile; kukimbia na kupiga mpira, huweza kuvua nguo na kuanza kutamka maneno kama mimi, wewe yule na kadhalika.

11. MIAKA MITATU(3) BAADA YA MTOTO KUZALIWA

Umri wa miaka mitatu tayari mabadiliko makubwa yameshatokea mwilini na bado yanazidi kutokea hapa mtoto anazidi kua mkubwa na kuanza kusimama kwa mguu mmoja, kukimbia zaidi, kujua jinsia na umri wake, huweza kuvaa na kuvua nguo lakini hawezi kufunga vifungo, anaweza kuhesabu moja mpaka kumi kama akifundishwa, anaweza kuruka na kuchora duara.

12. MIAKA MINNE(4) BAADA YA MTOTO KUZALIWA

Mtoto mwenye umri wa miaka minne huweza kufanya mambo mengi zaidi ikiwa ni pamoja na kuweza kusimulia kitu kilichomtokea,kufunga vifungo vya shati mwenyewe,kuweza kutumia choo mwenyewe na kwenda kujisaidia bila shida yoyote, Kuweza kucheza michezo mingi zaidi, kuweza kuruka kwa mguu moja bila kuanguka n.k.

13. MIAKA MITANO(5) BAADA YA MTOTO KUZALIWA

Katika umri huu wa miaka mitano; mtoto anaweza kuzitambua rangi nne za msingi, anaweza kuendesha baiskeli, anaongea kama watu wengine bila kuchanganya wakati uliopo na ujao,uelewa na akili yake kuzidi kukua zaidi pamoja na kufanya mambo mengine mengi sana.

Hizo ndyo baadhi ya Hatua za Ukuaji wa mtoto toka anazaliwa mpaka anapofikisha umri wa miaka mitano

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.