MWANAMKE Fanya Uchunguzi wa Saratani ya Mlango wa Kizazi Mara Kwa Mara
MWANAMKE Fanya Uchunguzi wa Saratani ya Mlango wa Kizazi Mara Kwa Mara,
Faida za Kufanya Uchunguzi wa Saratani ya mlango wa Kizazi (Cervical cancer Screening) mara kwa mara ni kubwa mno kwa Wanawake,
Kufanya Checkup kama hizi mara kwa mara itamsaidia Mwanamke ambaye tayari ana Saratani ya Mlango wa Kizazi kugundulika mapema na kupata Tiba,
KUMBUKA: Ni rahisi kupata Tiba na kupona kabsa kama Saratani ya mlango wa Kizazi(Cervical cancer) imegundulika mapema na Kuanza tiba mapema.
Wanawake ambao wapo Kwenye Hatari ya Kupata saratani ya shingo ya Kizazi,
Kwa Ujumla wanawake wote wapo kwenye hatari ya Kupata Saratani ya shingo ya Kizazi, ila kundi hili hapa Chini Lipo kwenye hatari zaidi.
KUNDI LILILOPO KATIKA HATARI YA KUPATA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI
➖ Wanawake Wenye Maambukizi ya Ukimwi(HIV/AIDS) au wanawake wenye magonjwa yoyote ambayo huweza kuathiri mfumo wa Kinga ya Mwili
➖ Wanawake wanaoshambuliwa na Kirusi cha Human papilloma virus(HPV) mara kwa mara
➖ Wanawake wanaovuta Sigara
➖ Wanawake wanaozaa watoto wengi
➖ Wanawake wanaotumia vidonge vya Uzazi wa Mpango(birth control Pills) Kwa Muda Mrefu zaidi, Mfano Kwa Miaka 3,5 au Zaidi.
DALILI NA VIASHIRIA VYA KUWA NA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI.
Chanzo cha Saratani ya Shingo ya Kizazi
Saratani ya shingo ya kizazi katika hatua za awali haina dalili au viashiria vyovyote.
– Kutokwa na damu katika tupu ya mwanamke (vagina) ambayo sio ya kawaida. Damu hii inaweza kuwa matone, au damu inayotoka katikati ya mzunguko wa hedhi (yaani baada ya hedhi kabla ya hedhi inayofuata) au damu itokayo kwa mwanamke ambae ameacha kupata hedhi.
– Kutokwa na damu baada ya kujamiana baada ya tendo la ndoa.
– Maumivu wakati wa kujamiana.
Dalili za saratani iliyosambaa ni kama zifuatavyo
– Kutokwa na majimaji ukeni kusiko kawaida yenye harufu na maumivu ya tumbo chini ya kitovu.
– Kupungua kwa hamu ya kula
– Kupungua uzito
– Kuhisi uchovu
– Maumivu ya nyonga
– Maumivu kwenye mgongo
– Maumivu ya mguu
– Mguu mmoja kuvimba
– Kutokwa na damu nyingi kwenye tupu ya mwanamke
– Kuvunjika mifupa (bone fractures)
– Kutokwa na mkojo au kinyesi kwenye tupu ya mbele ya mwanamke.