Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Jamii yaaswa kurudi kwenye Maadili yanayozingatia Mila na Desturi

Jamii yaaswa kurudi kwenye Maadili yanayozingatia Mila na Desturi.

VIONGOZI WA DINI, WAHARIRI WAFUNGUKA SABABU ZA MMOMONYOKO WA MAADILI.

Na WMJJWM, Dar Es Salaam.

Viongozi wa Dini, Wahariri wa Habari na Wadau mbalimbali wamebainisha sababu zinazochangia mmomonyoko wa maadili nchini na kuiasa jamii kurudi kwenye Maadili yanayozingatia Mila na Desturi.

Hayo yameelezwa wakati wa kikao cha Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima na Viongozi hao kwa lengo la kujadili changamoto ya Mmomonyoko wa Maadili katika kikao hicho kilichofanyika tarehe 24 Aprili, 2023 jijini Dar Es Salaam.

Wadau hao wakijadili mada zilizowasilishwa kuhusu maadili, wamesema malezi ya sasa yana changamoto kutokana na utandawazi, ukuaji wa teknolojia na wazazi kushindwa kuwajibika.

Akizungumza kwa niaba ya Jukwaa la Wahariri, Mwenyekiti wa Jukwaa hilo Bakari Machumu ameipongeza Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa kutafuta suluhisho na kulichukulia suala la maadili kwa uwazi ndani ya jamii.

“Kuwakutanisha Wahariri na vyanzo vya taarifa na elimu ambao ni viongozi wa Dini na Wadau wengine katika kikao hiki kitatupa fursa ya kwenda mbele zaidi kwani jukumu letu kuhakikisha tunapohabarisha tunaufahamu na kitu hicho. Umetujengea mahusiano na watoa taarifa” amesema Bakari Machumu.

Kwa upande wake Mchungaji mstaafu na Mkurugenzi wa Taasisi ya Hananja Compassion Foundation, Richard Hananja amesema majadiliano hayo yamekuja kwa wakati muafaka kutafuta suluhisho la changamoto ya maadili katika jamii.

“Watu wanakwenda kwenye nyumba za Ibada, tutumie nyumba za ibada hasa kwa Waumini wa Dini na Madhehebu mbalimbali kutoa elimu ya maadili kwa jamii” amesema Mchungaji Hananja.

Naye Shekh Rashid Shemzigwa aliyezungumza kwa niaba wa shekh wa mkoa wa Dar es Salaam, amesema kuwe na muda wa kutosha wa kujadili masuala ya maadili kwa Wadau wote Ili kuhakikisha changamoto ya mmomonyoko wa maadili inahubiriwa kila mahali.

Akifungua kikao hicho Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt Dorothy Gwajima amebainisha kuwa lengo la kikao hicho ni kuhakikisha ajenda ya maadili inamilikiwa na jamii yenyewe Ili kurudi kwenye utamaduni uliokuwepo hapo awali.

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.