Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

Tatizo la maumivu ya korodani,chanzo,dalili na Tiba

Tatizo la maumivu ya korodani,chanzo,dalili na Tiba

Katika Makala hii tumechambua Zaidi kuhusu chanzio cha Tatizo la Maumivu ya Korodani,tatizo ambalo huweza kumpata Mwanaume yoyote.

Tatizo la maumivu ya korodani

Tatizo la maumivu ya korodani linaweza kuwa la muda mfupi(acute) au likawa tatizo endelevu(chronic), hii ni kulingana na chanzo husika cha tatizo hili,

Na hapa tumeelezea Sababu mbali mbali za Tatizo la maumivu ya korodani

Chanzo cha Tatizo la maumivu ya korodani

Zipo Sababu mbali mbali ambazo huweza kupelekea mtu kupata Tatizo la maumivu ya korodani ikiwemo;

1. Kuharibiwa kwa Nerves kutokana na magonjwa mbali mbali kama vile Ugonjwa wa Kisukari(Diabetic neuropathy)

2. Mtu kupata ajali au Kuumia(Trauma/ injury) eneo la Korodani, Hii pia huweza kusababisha Tatizo la maumivu ya korodani

3. Kupata tatizo la Uvimbe kwenye Korodani, tatizo la Epididymitis n.k

4. Kupata tatizo la Busha au Hydrocele, tatizo la maji kujaa na kusababisha kuvimba kwa korodani

5. Kupata tatizo la Hernia hasa aina hii ya Inguinal hernia

6. Kupata tatizo la Mawe kwenye figo yaani Kidney stones, Hata hii pia huweza kusababisha Tatizo la maumivu ya korodani

7. Kupata tatizo la maambukizi au Kuvimba kwa tezi dume(Prostatitis)

8. Kupata maambukizi ya magonjwa mbali mbali kama vile UTI n.k,

maambukizi haya ya magonjwa huweza kupelekea mtu kupata Tatizo la maumivu ya korodani

9. Kupata tatizo la Testicular torsion (twisted testicle)

10. Kupata tatizo la kuvimba au kupanuka kwa mishipa ya veins ndani ya Korodani(Varicocele),

vyote hivi huweza kupelekea mtu kupata Tatizo la maumivu ya korodani

11. Pia Tatizo la maumivu ya korodani huweza kusababishwa na magonjwa mbali mbali ya Zinaa(Sexual transmitted diseases-STD’s) kama vile;Ugonjwa wa chlamydia

12. Tatizo la gangrene, ambapo tissue mbali mbali za mwili hufa, kutokana na Sababu mbali mbali ikiwemo;

FAQs: Maswali ambayo huulizwa mara kwa mara

Je,Uvimbe kwenye Korodani huweza kusababisha Tatizo la maumivu ya korodani?

Ndyo,Moja ya Sababu za mtu kupata Tatizo la maumivu ya korodani ni pamoja na kuwa na Uvimbe ndani ya Korodani,kuvimba kwa vimishipa vidogo kwenye eneo hili n.k

Hitimisho

Tatizo la maumivu ya korodani ni tatizo ambalo huweza kumpata Mwanaume yoyote,

Zipo Sababu mbali mbali zinazopelekea mtu kupata Tatizo la maumivu ya korodani,sababu hizo ni pamoja na;

Mtu kuumia eneo la korodani,kuharibiwa kwa nerves kutokana na magonjwa mbali mbali kama vile Kisukari, kuwa na Uvimbe kwenye korodani,maambukizi ya magonjwa ya Zinaa kama vile chlamydia,

Mwanaume kupata tatizo la kutanuka kwa mishipa ya Veins kwenye korodani kwa kitaalam hujulikana kama “Varicocele”, kupata maambukizi au Kuvimba kwa Tezi Dume n.k

Ukiona unapata Tatizo la maumivu ya korodani,hakikisha unaongea na wataalam wa afya ili kujua chanzo ni nini,na kisha kupata msaada wa matibabu mapema.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

2 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.