#Kandanda: Kiungo wa Manchester City Rodri amesema klabu hiyo bado ina hamu ya kushinda mataji zaidi
#Kandanda: Kiungo wa Manchester City Rodri amesema klabu hiyo bado ina hamu ya kushinda mataji zaidi wakati wanapojiandaa kumenyana na Sevilla kwenye fainali ya Kombe la UEFA Super Cup.
Vijana wa Pep Guardiola hata hivyo watazikosa huduma za nyota wao Kevin de Bruyne ambaye atakuwa nje kwa muda wa miezi minne kutokana na jeraha la msuli wa nyuma ya paja.
Fainali hiyo itachezwa katika uwanja wa Georgios Karaiskakis ulioko katik mji wa bandari wa Ugiriki wa Piraeus.
Unauonaje mchezo huo wa fainali? Tuandikie ubashiri wako.