Kundi la Taliban: Mwanamke akiwa uso wazi thamani yake inashuka
Kundi la Taliban limewahimiza Wanawake nchini Afghanistan kufunika nyuso zao wakiwa nje ya nyumba zao huku likisema Mwanamke akiwa uso wazi thamani yake inashuka.
@DW_Kiswahili imeripoti kuwa Msemaji wa Wizara muhimu katika Serikali ya Taliban huko Afghanistan amesema Wanawake hupoteza thamani pale Wanaume wanapoziona nyuso zao zilizofunuliwa hadharani.
Amesema kidini Wasomi nchini humo wanakubaliana kwamba Mwanamke ni lazima afunike uso wake akiwa nje ya nyumba.
Molvi Mohammad Sadiq Akif, Msemaji wa Wizara ya Taliban yenye kuhusika na masuala ya jamii amesema ikiwa nyuso za Wanawake zitaonekana hadharani kuna uwezekano wa kusababisha fitina au kuanguka katika dhambi.