Mafuriko nchini India yamesababisha,vifo vya takriban watu 24
Mafuriko nchini India yamesababisha,vifo vya takriban watu 24, tisa kati yao wamepoteza maisha kufuatia kuporomoka kwa hekalu la ibada nchini humo,
Na watu wengine chungunzima inakhofiwa hawajulikani waliko baada ya mvua kubwa kusababisha mafuriko na maporomoka ya ardhi.
Mvua za siku kadhaa zimesababisha mafuriko yaliyosomba magari,majumba kuporomoka na kuvunjika kwa madaraja katika majimbo ya kaskazini ya Uttarakhand na Himachal Pradesh,
Hali ya mafuriko na maporomoko ya ardhi sio kitu kigeni katika maeneo hayo na husababisha uharibifu mkubwa katika msimu wa masika lakini wataalamu wanasema mabadiliko ya tabia nchi yameongeza kasi ya hali hiyo pamoja na athari.
Source: DW