Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Serikali ya Ufaransa imetangaza kusitisha msaada wa fedha kwa Taifa la Burkina Faso

Serikali ya Ufaransa imetangaza kusitisha msaada wa fedha kwa ajili ya maendeleo na msaada wa fedha za bajeti kwa Taifa la Burkina Faso mara baada ya Nchi hiyo kutangaza kuunga mkono Mapinduzi yaliyofanyika nchini Niger.

AFP wameripoti kuwa uamuzi wa Ufaransa unakuja baada ya Burkina Faso na Mali kutangaza kuwa zinaunga mkono kitendo cha Wanajeshi kumpindua Rais wa Niger huku zikisema endapo ECOWAS itaivamia Niger ili kumrudisha Rais madarakani basi na wao watatangaza vita na ECOWAS na watapigana kuisaidia Niger.

Msaada wa Ufaransa kwenye maendeleo ya Burkina Faso unakadiriwa kuwa ni USD mil 530 na msaada wa Ufaransa kwenye bajeti ya Burkina Faso kwa mwaka jana ulikuwa ni Euro mil 13.
#MillardAyoUPDATES

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.