Kampeni Maalum Ya Utoaji Wa Chanjo Ya Matone Dhidi Ya Ugonjwa Wa Polio
Kampeni Maalum Ya Utoaji Wa Chanjo Ya Matone Dhidi Ya Ugonjwa Wa Polio.
Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na Wadau wa Chanjo imeandaa Kampeni Maalum ya utoaji wa chanjo ya matone kwa watoto chini ya umri wa miaka 8 dhidi ya ugonjwa wa Polio kwa lengo la kukinga na kuzuia maambukizi ya ugonjwa wa Polio kwa watoto kutokana na mwingiliano wa kijamii baina ya Tanzania na nchi jirani zenye mlipuko wa Polio.
Kampeni hii itafanyika katika mikoa ya Rukwa, Katavi, Songwe, Mbeya, Kigoma, Kagera kuanzia TAREHE 21 -24 Septemba 2023.