Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Tanzania yakopeshwa Bilioni miasaba kutoka Benki ya Dunia kuboresha Sekta ya Kilimo

Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema Tanzania imepata mkopo wa Dola Milioni miatatu za Kimarekani sawa na zaidi ya shilingi Bilioni miasaba kutoka Benki ya Dunia, fedha zitakazotumika kwa ajili ya kuboresha sekta ya Kilimo nchini.

Akizungumza mkoani Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Programu ya Uvumilivu wa Mifumo ya Chakula Tanzania Waziri Bashe amesema, Programu hiyo imepangwa kutekelezwa kwa muda wa miaka mitano, hivyo ataweka jitihada zaidi ikamilike ndani ya miaka mitatu.

Ameongeza kuwa fedha hizo zitaelekezwa katika kujenga miundombinu ya umwagiliaji kwenye maeneo walipo Wakulima wadogo.

Aidha, Waziri Bashe amesema moja ya matokeo ya programu hiyo ni kujenga miundombinu ya umwagiliaji kwa zaidi ya hekta elfu 37 na hivi sasa wizara hiyo imekwishaanza upembuzi yakinifu kwa ajili ya programu hiyo.

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.