Waziri Mkuu ameshiriki sherehe za uapisho za Rais mteule wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameshiriki sherehe za uapisho za Rais mteule wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa zilizofanyika katika uwanja wa Harare, Zimbabwe.
Rais Mnangagwa ameshinda uchaguzi huo kwa kura zaidi ya milioni 2.3 kati ya kura milioni 4.4 zilizopigwa sawa na asilimia 52.6 dhidi ya mpinzani wake Nelson Chamisa ambaye alipata kura milioni 1.9 sawa na asilimia 44.
Ushindi huo unamfanya Mnangagwa kuongoza nchi hiyo kwa kipindi cha pili cha miaka mitano.
Waziri Mkuu Majaliwa amemwakilisha Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan katika uapisho huo.