Mfahamu Andrea Lanfri aliyekatwa miguu kutokana na homa ya uti wa mgongo
Mfahamu Andrea Lanfri aliyekatwa miguu kutokana na homa ya uti wa mgongo.
Andrea Lanfri kijana aliyepatwa na ugonjwa wa meningitis akiwa na umri wa miaka 29 aliweza kupanda Mlima Everest licha ya kutokuwa na Miguu.
Anasema;
“Nilimshinda Everest baada ya kupoteza viungo vyangu kutokana na homa ya uti wa mgongo.”
“I conquered Everest after losing my limbs to meningitis.”
Andrea Lanfri alikuwa na umri wa miaka 29 alipopatwa na #meningitis, ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo.”
Alipata aina ya sumu kwenye damu iliyosababishwa na bakteria meningococcal kundi B na alipoteza fahamu kwa mwezi mmoja na nusu,
Alipozinduka, alikuwa na maumivu makali kwa miezi kadhaa ambapo aliweza kupata nafuu baada miguu yake yote miwili na vidole saba vilipokatwa.
Ili kupata nafuu zaidi ilimbidi “kujifunza upya jinsi ya kufanya kila kitu tangu mwanzo,mfano; kuandika, kula, kutembea n.k”
Licha ya changamoto hizo, anasema “mara moja aliona hii kuwa changamoto ya kurejea katika maisha yake yakawaida. Sikukata tamaa hata nilipoanguka: niliinuka na kujaribu kuelewa nilipoanguka nilikosea nini.”
Kwa mawazo haya aliendelea kushinda na kuweza kupanda Mlima Everest: