Tulitengana tangu 2016,Jada Pinkett Smith ameweka wazi
Jada Pinkett Smith ameweka wazi kuwa yeye na mumewe Will Smith wametengana tangu 2016.
Ingawa waigizaji hawa walikuwa wakiishi maisha tofauti kabisa kwa miaka saba, hawakuwa tayari kuthibitisha hadharani, alikiri katika mahojiano na kituo cha NBC.
Wanandoa bado wanaishi tofauti, lakini hawana mpango wa talaka.
Kulikuwa na uvumi juu ya ndoa yao mwaka 2020 baada ya Jada kupitia kipindi chake cha Red Table Talk kujadili “uhusiano” wake na msanii August Alsina.
Waigizaji hao waliokutana mwaka 1994 na kuoana mwaka 1997, wana watoto wawili waliozaa pamoja na mmoja Trey Smith, mtoto wa Smith na mke wake wa kwanza
#JadaPinkettSmith #willsmith