Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Breaking!! Wafukuzwa kazi Kisa uvamizi wa JELA

Zaidi ya wanajeshi 60 na Maafisa wa Magereza wamefukuzwa kazi nchini Guinea, kufuatia uvamizi wa jela uliofanyika Jumamosi huku Kiongozi wa zamani wa kijeshi, Moussa Dadis Camara, na wengine wawili wakikamatwa na kurejeshwa gerezani baada ya tukio hilo.

Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji la Serikali la RTG, limesema Maafisa waliofukuzwa kazi ni pamoja na Claude Pivi, Moussa Thiegboro Camara na Blaise Goumou na hadi sasa, mtoro Claude Pivi hajulikani alipo.

Kiongozi wa sasa, Kanali Mamadou Doumbia ametoa taarifa akisema kuwa walichukua hatua hiyo kutokana na “ukiukaji wa sheria za ajira na utovu wa nidhamu”.

Hata hivyo, tukio hili limeelezwa kama jaribio la kuhujumu mageuzi ya Serikali na jeshi limeapa kudumisha utulivu.

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.