Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

Vyakula Bora na Vibaya Zaidi kwa Ini Lako

Vyakula Bora na Vibaya Zaidi kwa Ini Lako

Hapa tumefanya uchambuzi wa baadhi ya vitu vya kufanya na kuzingatia, pamoja na vitu vya kuepuka kwa afya ya Ini lako, Pia kuna baadhi ya vyakula vya kuepuka na vingine vya kuvizingatia zaidi ili kuwa na Ini lenye afya bora.

1. Epuka kabsa vyakula vya mafuta mengi

Kula vyakula vingi sana vyenye mafuta mengi inaweza kufanya iwe vigumu kwa ini kufanya kazi yake. Baada ya muda inaweza kusababisha kuvimba kisha kupelekea Ini kuwa na kovu au tatizo ambalo kwa kitaalam linajulikana kama cirrhosis.

2. Kahawa(Coffee)

Kunywa kahawa kwa kiasi. Baadhi ya tafiti zinaonyesha kwamba kunywa vikombe viwili hadi vitatu kwa siku kunaweza kulinda ini lako kutokana na uharibifu unaosababishwa na pombe nyingi au mlo usiofaa.

Pia kuna Utafiti mmoja ulionyesha kuwa kahawa inaweza kupunguza hatari ya kupata saratani ya ini(Liver cancer).

3. Epuka kula vitu vyenye Sukari nyingi

Sukari nyingi sana zinaweza kuathiri ini lako. Hiyo ni kwa sababu moja ya kazi ya Ini ni kubadilisha sukari kuwa mafuta.

Ukizidisha, ini lako hutengeneza mafuta mengi, ambayo huishia kuning’inia mahali pasipohusika,

Ikiwa Kwa muda mrefu, unaweza kupata magonjwa kama vile ugonjwa wa mafuta kwenye ini kwa kitaalam fatty liver disease.

Kwa hivyo unaweza kulinda afya ya ini lako kwa kuepuka matumizi ya sukari nyingi.

4. Matumizi ya chai ya kijani(Green Tea)

Chai hii ina aina ya antioxidant inayofahamika kama catechins. Tafiti zinaonyesha kwamba catechins huweza kukulinda na Saratani mbali mbali ikiwemo Saratani ya Ini.

Hivo matumizi ya green tea ni bora kwa afya ya Ini.

5. Unywaji wa maji ya kutosha

Moja ya njia bora sana ya kutunza afya ya Ini lako ni kuhakikisha unakunywa maji ya kutosha kila siku,

Jenga Tabia ya kunywa maji badala ya vinywaji vilivyotiwa sukari nyingi kama vile soda, hii ni bora zaidi kwako.

9. Matumizi ya Karanga

Tafiti zinaonyesha kwamba, karanga zina virutubisho vya kutosha ikiwemo vitamin E,

Virutubisho hivi huweza kulinda Ini dhidi ya magonjwa kama vile ugonjwa wa mafuta kwenye ini kwa kitaalam fatty liver disease.

10. Matumizi ya mboga za majani ikiwemo Spinach

Mboga za majani zina antioxidant inayofahamika kama glutathione, ambayo inaweza kusaidia ini lako kufanya kazi vizuri.

11. Epuka kabsa matumizi ya Pombe au kunywa kwa kiasi kidogo sana(Be Moderate With Alcohol)

Kunywa kupita kiasi kunaweza kuharibu ini lako. Baada ya muda inaweza kusababisha tatizo la cirrhosis.

Hata unywaji wa kupindukia mara kwa mara ni hatari kwa afya yako —  Kunywa vinywaji vinne kwa mara moja kwa wanawake na vitano kwa wanaume — vinaweza pia kuwa na madhara.

Jaribu kujiwekea kikomo cha kunywa mara moja kwa siku ikiwa wewe ni mwanamke au mbili kwa siku ikiwa wewe ni mwanaume.

12. Punguza kula Vyakula Vilivyofungwa

Mara nyingi vyakula ambavyo ni packed foods vinakuwa na Kiwango kikubwa cha sukari,chumvi,mafuta n.k, Vitu hivi ni hatari kwa afya ya Ini lako.

13. Epuka matumizi ya kupita kiasi kwa baadhi ya dawa kama vile Acetaminophen

Acetaminophen Inapatikana katika dawa zaidi ya 600, pamoja na dawa nyingi za baridi na mafua. Watu wazima wengi hawapaswi kupata zaidi ya miligramu 4,000 kwa siku. Zaidi inaweza kuleta madhara kwenye ini lako.

14. Fanya ngono Salama jikinge na magonjwa ya Zinaa

Unataka kujilinda  wewe na mwenza wako dhidi ya hali zinazoweza kuenea kwa njia ya ngono, ikiwa ni pamoja na nyingi ambazo hatimaye zinaweza kuumiza ini lako.

Moja ni, Ugonjwa wa homa ya Ini-hepatitis C, B n.k, huambukiza moja kwa moja na inaweza kuleta madhara makubwa. Watu wengi hawatambui kuwa wana ugonjwa huu hadi miaka mingi baadaye wakati uharibifu mwingi umefanywa. Daktari wako anaweza kupima ili kuona kama unayo, hivo fanya vipimo.

15. Hakikisha unadhibiti shida ya uzito Mkubwa

Hiyo inamaanisha kufanyia kazi zaidi Uzito wako ili kuweka index ya uzito wa mwili (BMI) kuwa kati ya 18 na 25.

Mazoezi na mlo kamili ndio njia bora zaidi ya kukusaidia kudumisha uzito unaokufaa na kupunguza uwezekano wa kupata ugonjwa wa ini. Daktari wako anaweza kukusaidia kuweka mikakati ya kupunguza uzito ambayo itasaidia kuweka mwili wako mzima vizuri kwa muda mrefu.

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.