Wazazi tusiwalazimishe watoto wetu kusoma udaktari-Waziri Ummymwalimu
“Kila mtarajali (intern) anataka kubaki Mkoa wa Dar es Salaam, tunataka kuona watarajali pia wanakwenda katika Mikoa mingine, watarajali hawa ni muhimu sana katika kutoa huduma ” Waziri @ummymwalimu
“Watarajali (interns) waliofeli mtihani wanatakiwa kurudia mtihani hiyo kadri ya miongozo ya Baraza la Madaktari la Tanganyika (MCT) inavyoelekeza. Mtarajali anaweza kurudia mtihani mara tatu na akifeli mara zote anatakiwa kurudi ‘Internship’ kwa muda wa miezi sita” Waziri @ummymwalimu
“Wazazi tusiwalazimishe watoto wetu kusoma udaktari, tuwaache watoto wenyewe wapende maana udaktari ni kazi ambayo mtu anatakiwa aipende mwenyewe” Waziri @ummymwalimu